Mungu ni mwenye hekima na analeta maangamizi. Habadilishi masemi yake; lakini yuko tayari kuwaazibu watu waovu vilevile na wasaidizi wa watenda mabaya.
Musome katika kitabu cha Yawe: Hakuna hata kiumbe kimoja kitakachokosekana, kila kimoja kitakuwa na mwenzake. Maana kinywa cha Yawe kimeamuru hivyo. Roho yake itawakusanya hao wote.
Juu ya Kedari na falme za Hazori ambazo Nebukadneza mufalme wa Babeli alizishambulia na kuzishinda, Yawe anasema hivi: Simama uende kulishambulia kabila la Kedari! Uwaangamize watu wa mashariki!
Babu zenu hawakupata azabu kwa sababu ya kukataa maagizo yangu na amri nilizowapa kwa njia ya watumishi wangu manabii? Wakati huo, wao waligeuka na kusema kwamba: Yawe wa majeshi alikusudia kututendea kulingana na mienendo yetu na matendo yetu, na kweli ndivyo alivyotutendea.