Lakini sasa Yawe anasema hivi: Nyuma ya miaka mitatu kamili, ikihesabiwa kama vile mutumishi anavyohesabu siku zake, utukufu wa Moabu utapunguka. Ingawa watu wake ni wengi, watakaobaki wazima watakuwa wachache na wazaifu.
jangwa na miji yake yote vipige kelele, vijiji vya wakaaji wa Kedari vimusifu, wakaaji wa Sela waimbe kwa shangwe; wapige kelele kutoka juu kwenye mulima.
Makundi ya nyama wa inchi ya Kedari yatakusanyika kwako, utaweza kuwatumia kondoo dume wa Nebayoti; utatoa sadaka inayokubaliwa kwenye mazabahu ya Mungu, naye ataitukuza nyumba yake tukufu.
Juu ya Kedari na falme za Hazori ambazo Nebukadneza mufalme wa Babeli alizishambulia na kuzishinda, Yawe anasema hivi: Simama uende kulishambulia kabila la Kedari! Uwaangamize watu wa mashariki!