Mataifa yananguruma kama ngurumo ya maji mengi, lakini Mungu atayakaripia, nayo yatakimbilia mbali. Yatafukuzwa kama maganda juu ya mulima mbele ya upepo; kama mavumbi yanayonyanyuliwa na upepo mukali.
Wakubwa wenu wote walikimbia, wakakamatwa hata mbele ya kufyatua mushale mumoja. Watu wako wote waliopatikana walitekwa, ingawa walikuwa wamekimbilia mbali.
Hapo Waasuria watauawa kwa upanga, lakini si upanga wa watu; wataangamizwa kwa upanga ambao ni zaidi ya ule wa wanadamu. Waasuria watakimbia na vijana wao watatumikishwa kazi za kitumwa.