Abrahamu alikuwa na habara aliyeitwa Ketura. Ketura alimuzalia Abrahamu: Simurani, Yokisanu, Medani, Midiani, Isibaki na Sua. Wana wa Yokisanu walikuwa: Seba na Dedani.
Hautakaliwa tena na watu hata kidogo, watu hawataishi humo katika vizazi vyote. Hakuna Mwarabu atakayesimamisha hema yake humo, wala muchungaji atakayechunga nyama wake humo.
Mukimbie, enyi wakaaji wa Dedani, mugeuke na kujificha ndani ya mapango! Maana nitawaletea maangamizi, enyi wazao wa Esau; wakati wa kuwaazibu umefika.
Watu wa Dedani walifanya biashara nawe. Inchi nyingi za kandokando ya bahari zilikuwa masoko yako makubwa. Watu wake walikuletea pembe za tembo na miti mizuri inayoitwa ebene kwa kununua vitu kwako.