Isaya 21:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Ujumbe wa Mungu juu ya jangwa kando ya bahari. Kama upepo mukali unaovuma kutoka kusini, washambulizi wanakuja kutokea katika jangwa, kutoka katika inchi ya kutisha.
Yawe atawahurumia tena watu wa Yakobo, atawachagua tena Waisraeli. Atawarudisha katika inchi yao wenyewe, na wageni watakuja na kukaa pamoja na watu wa Yakobo.
Shuka, uikae katika mavumbi, ewe bikira, binti wa Babeli! Ikaa chini pasipo kiti cha kifalme, ewe binti wa Wakaldea! Tokea sasa hautaitwa tena murembo wala mwenye kupendeza.
Mishale yao ni mikali sana, pinde zao zimevutwa tayari. Kwato za farasi wao ni ngumu kama mawe; mwendo wa magurudumu ya magari ni kama wa upepo mukali.
Nilipoangalia niliona upepo wa zoruba unavuma kutokea upande wa kaskazini: kulikuwa wingu kubwa lililozungukwa na mwangaza, na moto ulitokea humo mufululizo na katikati ya huo moto kulikuwa kitu kinachometameta kama shaba.
Nebukadneza mwenyewe pamoja na watu wake, taifa la hatari kuliko mataifa yote, watatumwa kuiangamiza inchi ya Misri. Watachomoa panga zao juu ya Misri na kuijaza inchi hiyo watu waliouawa.
Watu wa mataifa mengine ya hatari sana, wataukata na kuuangusha chini na kuulalisha chini. Matawi yake yataanguka chini kwenye mulima na kila pahali katika mabonde; yatavunjika na kulala chini katika mitelemuko yote. Watu wote wataondoka chini ya kivuli chake na kuuacha.
Wakati wa mwisho mufalme wa kusini atamushambulia mufalme huyo wa kaskazini. Lakini mufalme wa kaskazini atajibu mashambulio hayo kwa nguvu kama zoruba, akitumia magari ya vita, waaskari wapanda-farasi na mashua nyingi. Atashambulia inchi nyingi na kupita katika inchi hizo kama mafuriko ya maji.