Isaya 20:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Yawe akasema: Mutumishi wangu Isaya amekuwa akitembea uchi na bila viatu kwa muda wa miaka mitatu sasa, kama kitambulisho juu ya inchi za Misri na Kushi.
Maana mimi ni Yawe, Mungu wenu, Mungu Mutakatifu wa Israeli, Mwokozi wenu. Ninaitoa inchi ya Misri kwa ajili ya ukombozi wenu, ninaitoa Kushi na Seba kusudi muachwe huru.
Wakiwa wanakuona, ujibebeshe muzigo wako kwenye mabega na kuondoka wakati wa giza. Funika uso wako usiweze kuona unakwenda wapi. Ndivyo ninavyokufanya kuwa kitambulisho kwa Waisraeli.
Vita itakuja katika inchi ya Misri, na wasiwasi utakuwa katika inchi ya Etiopia, wakati Wamisri wengi wataanguka wameuawa, mali zao zitakaponyanganywa, na misingi ya miji yao kubomolewa.
Yawe anasema hivi: Wote wanaounga Misri mukono wataangamia, mashujaa wake wenye utukufu wataangamizwa, tangu Migidoli mpaka Sewene watu watauawa katika vita. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
Nawe utwae bamba la chuma. Ulisimamishe likuwe kama ukuta wa chuma kati yako na muji. Kisha utaelekezea muji huo uso wako nao utashambuliwa na utaushambulia. Hiki kitakuwa kitambulisho kwa taifa la Waisraeli.
Kutokana na makosa yenu, mutataabika kwa muda wa miaka makumi ine, sawa na zile siku makumi ine mulizopeleleza ile inchi, mwaka mumoja kwa kila siku moja; mutatambua kwamba mimi nimechukizwa.