Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 20:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Miaka mitatu mbele ya pale, Yawe alimwambia Isaya mwana wa Amozi hivi: Kwenda uvue nguo ya gunia uliyokuwa umevaa katika kiuno, na viatu vyako. Isaya akafanya kama alivyoambiwa; akakuwa anatembea uchi na bila viatu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 20:2
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Daudi aliendelea, akapanda kwenye mulima wa Mizeituni akilia, bila viatu na kichwa chake kimefunikwa. Hata watu wote waliokuwa pamoja naye walifunika vichwa vyao, wakapanda mulima wakilia.


Daudi aliporudi kwake kwa kuibariki jamaa yake, Mikali, binti ya Saulo, alikwenda kumupokea, akasema: “Ni ajabu kwa mufalme wa Waisraeli kujiheshimu leo, kwa kujifunua uchi wake mbele ya watumishi wake na wajakazi wake sawa vile mushenzi anavyovua nguo zake mbele ya watu bila haya!”


Wao wakamujibu: “Alikuwa akivaa nguo ya manyoya na mukaba wa ngozi kwenye kiuno.” Mufalme akasema: “Yule ni Elia wa Tisibe!”


Usikie, ee Yawe, unihurumie; ee Yawe, unisaidie!”


Yawe akamwambia: “Usikuje karibu! Vua viatu vyako kwa sababu pahali unaposimama ni pahali patakatifu.”


Haya ni maono Isaya mwana wa Amozi, aliyoyaona juu ya inchi ya Yuda na Yerusalema, katika nyakati za utawala wa wafalme hawa wa Yuda: Ahazi na Hezekia.


Haya ni maono, ambayo nabii Isaya mwana wa Amozi, aliyofunuliwa na Mungu juu ya inchi ya Babeli:


Aliwaamuru Eliakimu, musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna, katibu, na wazee wa makuhani, wamwendee nabii Isaya mwana wa Amozi, wakiwa wamevaa nguo za magunia.


Kila mutu amenyoa kichwa na ndevu zake. Wote wamejikatakata kwenye mikono na kwenye viuno wamevaa gunia.


Utaugua, lakini sio kwa sauti. Hautamufanyia kilio huyo aliyekufa. Vaa viatu vyako na kuvaa kitambaa; usiufunike uso wako wala kula chakula cha kilio.


Mutavaa vitambaa kwa kichwa na viatu; hamutaomboleza, wala kulia. Kutokana na maovu yenu, mutaregea na kuugua, kila mutu na mwenzake.


Yawe akaniambia tena: Wewe mwanadamu, twaa tofali, uliweke mbele yako na uchape juu yake muji, kama wa Yerusalema.


Nimekupangia muda wa siku mia tatu na makumi kenda. Muda huu ni sawa na miaka ya azabu yao: siku moja ni sawa na mwaka mumoja. Utabeba azabu ya Waisraeli kwa muda huu.


Enyi wakaaji wa Safiri, muende mukiwa uchi na wenye haya. Wakaaji wa Zanana musitoke inje ya muji wenu. Watu wa Beti-Ezeli wanalia; musaada wao kwenu umeondolewa.


Kwa sababu hiyo, mimi nitalia na kuomboleza; nitatembea uchi na bila viatu. Nitaomboleza na kulia kama mbweha, nitasikitika na kulia kama mbuni.


Siku hiyo, kila nabii atapata haya kwa ajili ya maono yake anapotabiri. Hawatavaa nguo za manyoya kwa kudanganya watu,


Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kama mutu akitaka kunifuata, ajikane yeye mwenyewe, lakini ajitolee kwa kubeba musalaba wake na kunifuata.


Yoane alikuwa akivaa nguo iliyotengenezwa na manyoya ya ngamia na mukaba wa ngozi katika kiuno. Naye alikuwa akikula nzige na asali ya pori.


Halafu mwanafunzi yule aliyependwa na Yesu akamwambia Petro: “Ni Bwana.” Simoni Petro aliposikia kwamba ni Bwana, akavaa kanzu yake (kwa maana alikuwa havai kitu), naye akajitupa ndani ya maji.


Na yule mutu aliyekuwa na pepo ndani yake akawarukia, akawashinda wote nguvu na kuwatendea vibaya hata wakakimbia toka nyumba yake wakiwa uchi na wakijaa vidonda.


Akatufikia, akatwaa mukaba wa Paulo, akajifunga miguu na mikono yake mwenyewe na kusema: “Roho Mutakatifu anasema: ‘Wayuda watamufunga mutu mwenye mukaba huu namna hii kule Yerusalema na kumutoa kwa watu wa mataifa mengine.’ ”


Huyo jemadari wa jeshi la Yawe akamwambia: “Vua viatu vyako kwa maana pahali unaposimama ni patakatifu.” Yoshua akafanya hivyo.


Nami nitawatuma washuhuda wangu wawili, wakiwa wamevaa nguo za kilio. Nao watatangaza ujumbe wa Mungu kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na makumi sita.”


Alivua nguo zake, akatabiri mbele ya Samweli. Alibaki uchi kwa siku moja, muchana na usiku. Kwa hiyo watu walianza kujiuliza: “Hata Saulo ni mumoja wa manabii?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ