Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 2:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Inchi yao imejaa sanamu za miungu, watu wake wanaabudu kazi ya mikono yao, vitu walivyotengeneza wao wenyewe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 2:8
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tena, neno la Yawe lilifika kwa njia ya nabii Yehu mwana wa Hanani juu ya Basha na jamaa yake, kwa sababu ya maovu aliyotenda mbele ya Yawe. Basha alimukasirikisha Yawe kwa matendo yake; alimwiga Yeroboamu na jamaa yake na kuiletea jamaa yake maangamizi.


Juu ya kila kilima na chini ya kila muti wenye majani mabichi, walijenga nguzo za mawe na sanamu za miungu wa kike Ashera,


Walivunja amri zote za Yawe, Mungu wao. Wakatengeneza sanamu za miungu ya wana-ngombe wawili wa madini yenye kuyeyushwa, wakatengeneza sanamu za Ashera, wakaabudu jeshi la mbingu, na wakamutumikia Bali.


Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe kama vile Uzia baba yake alivyotenda. Hakuingia katika hekalu la Yawe. Watu waliendelea kufanya maovu.


Hawataelekea tena mazabahu ambazo ni kazi za vidole vyao wenyewe, wala kuzitazamia tena kazi za mikono yao wenyewe, ni kusema sanamu za mungu Ashera na mazabahu za kufukizia ubani.


Ee Yawe, Mungu wetu, tulipata kutawaliwa na wabwana wengine ambao si wewe, lakini tunakubali wewe pekee kuwa Mungu wetu.


Walitupa miungu yao katika moto kwa sababu haikukuwa miungu ya kweli, lakini sanamu za miti na mawe zilizochongwa na mikono ya watu.


Anafanana na sanamu? Hiyo, fundi anaichonga, mufuaji wa zahabu anaipakaa zahabu, na kuitengenezea mukufu wa feza!


Miungu hiyo yote ni udanganyifu, haiwezi kufanya kitu chochote; sanamu zao ni upepo tu, hazina maana.


Ninyi munawaka tamaa kwenye miti ya mialo, na chini ya kila muti wenye kuwa na majani mabichi. Munawachinja watoto wenu na kuwatambikia katika mabonde na ndani ya nyufa za mawe.


Nami nitawahukumu Waisraeli kwa ajili ya uovu wao wote, kwa maana waliniacha mimi na kuifukizia miungu mingine ubani na kuabudu sanamu walizojitengenezea wenyewe.


Enyi watu wa Yuda, hesabu ya miji yenu ni sawasawa na hesabu ya miungu yenu. Na kama vile barabara zenu za Yerusalema zinavyokuwa nyingi, ndivyo mulivyojenga mazabahu ya haya, ni kusema ya kufukizia ubani kwa mungu Bali.


Lakini iko wapi ile miungu yenu muliyojifanyia? Basi kama inaweza, isimame iwasaidie, wakati munapokuwa katika shida. Ee ninyi watu wa Yuda, hesabu ya miungu yenu ni sawa na hesabu ya miji yenu!


Mimi niliongea na manabii; ni mimi niliyewapa maono mengi, na kwa njia yao nilitangaza mupango wangu.


Waefuraimu wanaendelea kutenda zambi, wanajitengenezea sanamu za feza yenye kuyeyushwa, sanamu zinazotengenezwa kwa ufundi wao, zote zikiwa kazi ya wafundi. Wanasema: Muzitambikie! Wanaume wanabusu sanamu ya mwana-ngombe!


Muombe huruma kwake, mumurudilie na kumwambia: Utusamehe uovu wote, upokee zawadi zetu, nasi tutakusifu kwa moyo.


Ile sanamu inatoka Israeli, ni fundi ndiye aliyeitengeneza. Yenyewe si Mungu hata kidogo. Kweli! Sanamu ya mwana-ngombe ya Samaria itavunjwavunjwa!


Nitaziharibu sanamu zenu, na nguzo zenu za ibada; nanyi mutakoma kuabudu vitu mulivyotengeneza wenyewe.


Paulo alipokuwa akingojea Sila na Timoteo kule Atene, moyo wake ukavunjika sana kuona namna muji ule ulivyojaa sanamu za miungu.


Huko mutatumikia miungu ya miti na mawe ambayo imetengenezwa kwa mikono ya watu na ambayo haiwezi kuona, haisikii, haikuli wala kunusa.


Watu waliobaki bila kuuawa na yale mapigo hawakuachana na sanamu walizojitengenezea wao wenyewe. Hawakuacha kuabudu pepo, sanamu za zahabu, za feza, za shaba, za mawe na za miti zisizoweza kuona, wala kusikia, wala kutembea.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ