Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 2:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Mungu atafanya hukumu kati ya mataifa; ataamua maneno kati ya watu wengi. Watu watafua panga za vita kuwa majembe na mikuki yao kuwa visu vya kuvuna. Taifa halitapigana na taifa lingine wala hayatafanya tena mazoezi ya vita.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 2:4
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Atayahukumu mataifa na kuwaua watu wengi; atawaponda waongozi kila nafasi katika dunia.


Anakomesha vita popote katika dunia. Anavunjavunja pinde na mikuki, nayo magari ya vita anayateketeza.


Mukuje muone matendo ya Yawe. Muone maajabu aliyofanya katika dunia.


Simama sasa, ee Mungu, uuhukumu ulimwengu; maana mataifa yote ni mali yako.


mbele ya Yawe kwa sababu anakuja. Anakuja kuhukumu dunia. Atahukumu dunia kwa haki, na mataifa kwa uaminifu wake.


Kutokana na kutenda kwa haki, watu watapata amani, utulivu na usalama kwa milele.


Watu wangu watakaa katika makao ya amani, katika pahali penye usalama na nafasi yenye utulivu.


Maana Yawe ni mwamuzi wetu, yeye ni mutawala wetu; Yawe ni mufalme wetu, yeye ndiye anayetuokoa.


Muangalie mutumishi wangu ninayemusaidia; muchaguliwa wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye. Nimeiweka roho yangu juu yake, naye ataimarisha sheria yangu katika mataifa.


Hatavunja tete lililokunjama, hatazimisha utambi unaotoa moshi; ataimarisha sheria yangu kwa uaminifu.


Maana mutoto amezaliwa kwa ajili yetu, tumepewa mutoto mwanaume. Naye atapewa mamlaka ya kutawala. Ataitwa: “Mushauri wa Ajabu”, “Mungu Mwenye Nguvu”, “Baba wa Milele”, “Mufalme wa Amani”.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Siku hiyo, wewe utaniita “Mume wangu”, na sio tena “Bali wangu”. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Nitafanya agano na nyama wa pori, ndege pamoja na vyote vinavyotambaa, kusudi wasikuumize. Nitaondoa upinde, upanga na silaha za vita katika inchi, na kukufanya uishi kwa usalama.


Mungu atatoa hukumu kati ya mataifa mengi, atakata mashauri ya mataifa makubwa ya mbali. Nayo yatafua mapanga yao kuwa majembe, na mikuki yao kuwa visu vya kuvuna. Taifa halitapigana na taifa lingine, wala hayatafanya tena mazoezi ya vita.


Ataondoa kabisa magari ya vita katika inchi ya Efuraimu, na farasi wa vita kutoka katika Yerusalema; pinde za vita zitatupwa mbali. Naye ataleta amani kati ya mataifa; utawala wake utaenea toka bahari mpaka bahari, toka muto Furati hata miisho ya dunia.


Kwa maana amekwisha kupanga siku atakapohukumu dunia kwa haki, kwa njia ya mutu mumoja, yule aliyemuweka kwa kazi ile. Naye amehakikisha mambo hayo kwa kumufufua mutu yule.”


Kisha nikaona mbingu imefunguka na kukatokea farasi mweupe. Yule aliyepanda juu yake anaitwa Mwaminifu na Mwenye Ukweli, kwa maana anahukumu na kupigana vita kwa haki.


Waadui za Yawe watavunjwa vipandevipande; atanguruma juu yao kama radi mbinguni. Yawe ataihukumu dunia yote, atamupa nguvu mufalme wake, na atautukuza uwezo wa muchaguliwa wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ