22 Usimutumainie mwanadamu, uzima wake ni kama pumzi tu. Yeye anafaa kitu gani?
Halafu Yawe Mungu akamwumba mwanaume kwa udongo, akamupulizia ndani ya pua pumzi ya uzima, na yule mwanaume akakuwa kiumbe chenye uzima.
kila kiumbe chenye uzima katika inchi kavu kilikufa.
ninaapa kwamba kadiri ninavyoweza kupumua, roho ya Mungu ikiwa bado ndani yangu,
Musiwategemee wakubwa wa dunia; hao ni wanadamu tu, hawawezi kuokoa.
Enyi watu, mutumainie Mungu siku zote; mumufungulie yanayokuwa ndani ya moyo wenu. Yeye ndiye kimbilio letu.
Nikiangalia mbingu uliyoumba kwa vidole vyako, mwezi na nyota ulizozisimika huko,
Kwake mataifa ni kama tone la maji katika mbeketi, ni kama mavumbi juu ya kilo. Kwake visanga ni vyepesi kama mavumbi laini.
Mataifa yote si kitu mbele yake; kwake ni vitu vya ovyo na bure kabisa.
Yawe anasema hivi: Mimi, kweli mimi, ndiye ninayekufariji. Kwa nini wewe unamwogopa mutu ambaye ni wa kufa, mwanadamu ambaye anatoweka kama majani?
Yawe anasema hivi: Alaaniwe mutu anayemutegemea mwanadamu, mutu ambaye anategemea nguvu za mwanadamu, mutu ambaye moyo wake umegeuka mbali nami Yawe.
Tunayoona sisi, ni kwamba wenye kiburi ndio wenye furaha siku zote. Watu waovu, ingawa wanastawi, hata wanapomujaribu Mungu, hawapati azabu.
Ninyi hamujui namna gani maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Kwa maana ninyi ni kama muvuke unaoonekana kwa wakati kidogo, kisha unatoweka.