Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 2:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kweli, siku ya Yawe wa majeshi inakuja juu ya wote wenye kiburi na majivuno, juu ya wote wanaojitukuza,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 2:12
42 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wewe unawaokoa wanyenyekevu, lakini unaangalia wenye majivuno kusudi uwashushe.


Mbona Mungu Mwenye Uwezo hapangi wakati wa hukumu? Kwa nini wanaomujua hawajui hizo siku zake?


Wimbo wa safari za kidini: wa Daudi. Ee Yawe, sina moyo wa majivuno; wala macho yangu si ya kiburi. Sijishugulishi na mambo makubwa, yale yanayokuwa ya ajabu sana kwangu.


Wewe unawaokoa wanyenyekevu, lakini unawashusha wenye macho ya kujivuna.


Lakini Yawe anamuchekelea mwovu, kwa maana anajua mwisho wake ni karibu.


Usimame, ee mwamuzi wa watu wote; uwaazibu wenye kiburi inavyowastahili!


Kila mwenye kiburi ni chukizo kwa Yawe. Hakika mutu wa namna hiyo hatakosa kuazibiwa.


Wakati Yawe atakapomaliza kazi zake zote kwenye mulima Sayuni na katika Yerusalema, atamwazibu mufalme wa Asuria, kwa sababu ya majivuno na kiburi chake.


Bwana, Yawe wa majeshi atakata matawi kwa ukali, miti mirefu itaangushwa chini, wanaokuwa juu watashushwa.


Yawe anasema hivi: Nitauazibu ulimwengu kwa uovu wake, waovu kwa sababu ya makosa yao. Nitakikomesha kiburi cha wenye majivuno, na kuporomosha mazarau ya watu wakali.


Mulie, maana siku ya Yawe imekaribia; inakuja kama uharibifu kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu.


Siku ya Yawe inakuja, siku kali, ya kasirani na hasira kali. Itaifanya inchi kuwa uharibifu, itawaangamiza wenye zambi ndani yake.


Lakini umeporomoshwa mpaka kuzimu; umeshushwa chini kabisa ndani ya shimo.


Ni Yawe wa majeshi! Yeye ndiye aliyeyapanga haya yote. Alifanya hivyo akiharibu kiburi chao na kuwapatisha haya waheshimiwa wake.


Siku ile Yawe ataliazibu jeshi la anga vilevile na wafalme wa dunia.


Dunia inakauka na kunyauka; ulimwengu unafazaika na kunyauka; mbingu zinafazaika pamoja na dunia.


Yeye anawashusha wakubwa wenye nguvu, anawafanya watawala wa dunia kuwa si kitu.


Nitaharibu milima na vilima, na majani yote nitayakausha. Mito ya maji nitaigeuza kuwa inchi kavu, na visima vya maji nitavikausha.


Kila mutu atafezeheshwa, na wenye kiburi wote watapatishwa haya.


Amenituma kutangaza mwaka wake wa neema, na siku ya Mungu wetu ya kulipiza kisasi kusudi niwafariji wote wanaoomboleza.


Urizi wangu umekuwa kama ndege muzuri ambaye anashambuliwa pande zote na ndege wakali? Muende kuwakusanya nyama wote wa pori, muwalete wakule.


Yawe anasema hivi: Hivi ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha watu Yuda na kiburi kikubwa cha watu wa Yerusalema.


Kweli, siku hiyo ni kubwa, hakuna ingine kama hiyo; ni siku ya taabu kwa watu wa Yakobo; hata hivyo, wataokolewa toka humo.


Lakini siku hiyo ni siku ya Bwana wetu Yawe wa majeshi. Ni siku ya kulipiza kisasi, siku ya kuwaazibu waadui zake. Upanga utawamaliza hao na kutosheka, utaikunywa damu yao na kushiba. Maana Bwana wetu Yawe wa majeshi yuko na sadaka huko kaskazini karibu na muto Furati.


Mimi, ninapigana nawe, ewe mwenye kiburi. –Ni ujumbe wa Bwana wa wote, Yawe wa majeshi.– Maana siku yako ya azabu imefika, wakati nitakapokuazibu umetimia.


Hawakwenda kulinda sehemu zile za kuta zilizobomoka wala hawajengi kuta mupya kusudi Waisraeli waweze kujilinda wakati wa vita siku ile ambayo mimi Yawe nimeiweka.


Ole kwenu ninyi munaoingojea kwa hamu siku ya Yawe! Kwa nini munaitaka sana siku hiyo? Siku hiyo, itakuwa siku ya giza na si ya mwangaza!


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninapanga kuwaletea ninyi hasara, ambayo hamutaweza kuiponyoka hata kidogo. Utakuwa wakati mubaya kwenu, wala hamutaweza kutembea kwa maringo.


Nitakomesha matendo yenu ya uchawi, nanyi hamutakuwa tena na waaguzi.


Siku hiyo ni ya mulio wa baragumu ya vita, juu ya miji yenye vikingio na kuta ndefu.


Siku hiyo, hautapata haya kutokana na matendo yako ya kuniasi, maana nitawaondoa kati yako wale wanaojivuna na kujitukuza, nawe hautakuwa na kiburi tena kwenye mulima wangu mutakatifu.


Na yeyote anayejiinua, atashushwa, lakini anayejishusha, atainuliwa.


Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Basi munapaswa kumutoa mutu yule kwa Shetani, kusudi mwili wake uharibiwe, nayo roho yake iweze kuokolewa Siku ile Bwana Yesu atakaporudi.


Kwa maana munajua ninyi wenyewe kwamba siku Bwana atakaporudia, itatimia kwa saa musiyozania kama vile mwizi anavyokuja usiku.


Lakini Mungu ametujalia neema kubwa zaidi, kwa maana Maandiko yanasema: “Mungu anapingana na wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ