Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 2:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Macho yenye kiburi ya wanadamu yatanyenyekezwa, watu wenye majivuno watashushwa chini, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 2:11
61 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wewe unawaokoa wanyenyekevu, lakini unaangalia wenye majivuno kusudi uwashushe.


bila kosa kwa wale ambao hawafanyi makosa, lakini mukali kwa waovu.


Wewe unawaokoa wanyenyekevu, lakini unawashusha wenye macho ya kujivuna.


Wamoja wanajivunia magari ya vita, wengine farasi wao. Lakini sisi tunajivunia Yawe, Mungu wetu.


Anakomesha vita popote katika dunia. Anavunjavunja pinde na mikuki, nayo magari ya vita anayateketeza.


Anasema: “Munyamaze na kujua kwamba mimi ni Mungu! Mimi ninatukuzwa katika mataifa yote; mimi ninatukuzwa katika ulimwengu wote!”


Usimame, ee mwamuzi wa watu wote; uwaazibu wenye kiburi inavyowastahili!


Kila mwenye kiburi ni chukizo kwa Yawe. Hakika mutu wa namna hiyo hatakosa kuazibiwa.


Kuna watu ambao macho yao yanajaa kiburi. Wanazarau kila kitu wanachoona.


Wakati Yawe atakapomaliza kazi zake zote kwenye mulima Sayuni na katika Yerusalema, atamwazibu mufalme wa Asuria, kwa sababu ya majivuno na kiburi chake.


Siku hiyo mutasema: Ninakushukuru, ee Yawe, maana ingawa ulinikasirikia, hasira yako imetoweka, nawe umenifariji.


Siku hiyo mutasema: Mumushukuru Yawe, muombe kwa jina lake. Mujulishe kwa mataifa matendo yake, mutangaze kuwa jina lake limetukuzwa.


Yawe anasema hivi: Nitauazibu ulimwengu kwa uovu wake, waovu kwa sababu ya makosa yao. Nitakikomesha kiburi cha wenye majivuno, na kuporomosha mazarau ya watu wakali.


Lakini umeporomoshwa mpaka kuzimu; umeshushwa chini kabisa ndani ya shimo.


Kiburi cha wanadamu kitashushwa, majivuno ya watu yatanyenyekezwa, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Ni Yawe wa majeshi! Yeye ndiye aliyeyapanga haya yote. Alifanya hivyo akiharibu kiburi chao na kuwapatisha haya waheshimiwa wake.


Siku ile Yawe ataliazibu jeshi la anga vilevile na wafalme wa dunia.


Siku ile, watu wote watasema: Huyu ndiye Mungu wetu! Tumemungojea atuokoe. Huyu ndiye Yawe tuliyemutazamia. Mukuje tufurahi na kushangilia kwa sababu ametuokoa.


Siku ile watu wataimba wimbo huu katika inchi ya Yuda: Sisi tuna muji imara: Mungu anatulinda kwa kuta na upango.


Siku ile Yawe wa majeshi atakuwa taji tukufu, kama kitambaa kizuri kwa watu wake watakaobaki wazima.


Siku hiyo viziwi watasikia ujumbe ukisomwa katika kitabu na kutoka katika giza, vipofu wataanza kuona.


Hata hivyo, Yawe anangoja kuwasamehe, atasimama na kuwaonea huruma. Yawe ni Mungu wa haki. Heri wote wale wanaomutumainia.


Mutakapopanda mbegu zenu, Yawe atanyesha mvua kwa wakati wake, nazo zitakomaa na kuwapa mavuno mengi mazuri. Makundi yenu ya nyama nao watakula katika mashamba makubwa ya kukulishia nyama.


Wewe umemutukana nani? Umemutusi nani? Umesubutu kumufokea nani kwa majivuno? Ni Mungu, Mutakatifu wa Israeli!


Wakati huo wanawake saba watashikamana na mwanaume mumoja na kumwambia: Chakula na mavazi tutajitafutia wenyewe, lakini wewe utuondolee haya yetu, uturuhusu tuitwe kwa jina lako.


Yeye anawashusha wakubwa wenye nguvu, anawafanya watawala wa dunia kuwa si kitu.


Kwa hiyo watu wangu watajua mimi ni nani. Siku hiyo watajua kwamba ni mimi ninayesema: “Niko!”


Urizi wangu umekuwa kama ndege muzuri ambaye anashambuliwa pande zote na ndege wakali? Muende kuwakusanya nyama wote wa pori, muwalete wakule.


Siku zinakuja ambapo nitawaazibu wote waliotahiriwa kimwili tu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Ni kusema nitawaazibu:


Kwa hiyo, ewe mwanadamu, toa unabii na kumwambia Gogi kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Siku ile, taifa langu la Waisraeli litaishi kwa usalama, wewe utafunga safari


Mimi ninasema wazi kwa wivu na kasirani yangu kali kwamba siku hiyo kutakuwa tetemeko kubwa la inchi katika inchi ya Israeli.


Katika siku ile, nitamupa Gogi pahali pa kufanyia maziko katika inchi ya Israeli, katika Bonde la Wasafiri, upande wa mashariki wa bahari ya Chumvi. Gogi atazikwa huko pamoja na kundi lake lote la waaskari, nao wasafiri watazuizwa kupita kule. Bonde hilo litaitwa, Bonde la Hamoni-Gogi.


Waisraeli watajua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wao, tangu siku hiyo na itakayokuja.


Na sasa, mimi Nebukadneza ninamusifu na kumutukuza na kumuheshimu Mufalme wa mbinguni. Maana matendo yake yote ni ya haki, naye anawashusha wenye kiburi.


Kwa hiyo, nitamushawishi, nitamupeleka katika jangwa na kusema naye kwa upole.


Siku hiyo, wewe utaniita “Mume wangu”, na sio tena “Bali wangu”. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Nitakufanya muke wangu milele; ukuwe wangu kwa sheria na haki, kwa wema na huruma.


Siku inakuja nitakapoisimika nyumba ya Daudi iliyoanguka; nitazitengeneza kuta zake, na kusimika upya mabomoko yake. Nitaijenga upya kama ilivyokuwa tangu zamani.


Mimi Yawe ninakuuliza hivi: Siku hiyo, sitawaangamiza wenye hekima kutoka Edomu na wenye maarifa kutoka mulima wa wazao wa Esau?


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninapanga kuwaletea ninyi hasara, ambayo hamutaweza kuiponyoka hata kidogo. Utakuwa wakati mubaya kwenu, wala hamutaweza kutembea kwa maringo.


Siku ile, nitawakusanya waliolemewa, nitawakusanya waliopelekwa katika uhamisho, watu wale ambao niliwaazibu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Nitaiharibu miji ya inchi yenu, na kubomoa vikingio vyenu.


Siku hiyo, hautapata haya kutokana na matendo yako ya kuniasi, maana nitawaondoa kati yako wale wanaojivuna na kujitukuza, nawe hautakuwa na kiburi tena kwenye mulima wangu mutakatifu.


Siku hiyo, Yerusalema utaambiwa: Usiogope, ee Sayuni, usilegee mikono.


Wakati ule, Yawe, Mungu wao, atawaokoa, maana wao ni kundi lake; nao watangaa katika inchi yake kama mawe ya bei kali katika taji.


Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Lakini, kama Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Anayetaka kujivuna, ajivune kwa ajili ya Bwana.”


kuangusha vizuizo vyote watu wanavyojivunia kwa kupinga elimu ya Mungu. Tunatawala mafikiri ya watu na kuyafanya yapate kumutii Kristo.


atakapokuja apate kutukuzwa na watu wake na kushangiliwa na wale wote wanaoamini. Ninyi vilevile mutakuwa pamoja nao kwa maana mumeamini habari tuliyowatangazia.


Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ