Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 2:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Muingie chini ya jiwe, mujifiche katika mavumbi, kwa kuepuka kitisho cha Yawe, mbali na mwangaza wa utukufu wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 2:10
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maana hasara kutoka kwa Mungu ni kitisho kwangu; mimi siwezi kusimama mbele ya ukubwa wake.


Uwazike wote pamoja ndani ya udongo; umufunge kila mumoja kwa kifungo cha kifo.


kusudi kila mutu ajue matendo yako makubwa, na mamlaka ya ufalme wako wenye utukufu.


Nani anayetambua uzito wa hasira yako? Nani anayeona matokeo ya kasirani yako?


Mutafanya nini siku ya azabu, siku zoruba itakapowakujia kutoka mbali? Mutamukimbilia nani kwa kuomba musaada? Mutakwenda wapi kwa kuweka mali yenu?


Watainyoosha mikono yao kama mutu anayejaribu kuogelea, lakini pamoja na bidii yao, Yawe ataporomosha kiburi chao.


Lakini hawa ni watu walioibwa mali yao na kunyanganywa! Wote wamenaswa katika mashimo, wamefungwa katika kifungo. Wamenyanganywa bila mutu wa kuwaokoa, wamekamatwa mateka na hakuna anayesema: Muwarudishe!


Lakini Yawe ni Mungu wa kweli, Mungu Mwenye Uzima, mufalme wa milele. Akikasirika, dunia inatetemeka, mataifa hayawezi kuvumilia hasira yake.


Nani asiyekuogopa wewe, ee mufalme wa mataifa? Wewe unastahili kuheshimiwa: kwa maana kati ya wenye hekima wote wa mataifa, na katika falme zao zote, hakuna hata mumoja anayekuwa kama wewe.


Yawe anasema hivi: Hivi ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha watu Yuda na kiburi kikubwa cha watu wa Yerusalema.


Pahali pa kutambikia juu ya vilima pa Aweni, pahali Waisraeli walipofanyia zambi, pataharibiwa. Miiba na michongoma vitaota katika mazabahu zao. Nao wataiambia milima: Mutufunike na vilima: Mutuangukie!


Ninawe, nawe vilevile utalewa; utamukimbia adui na kujaribu kujificha.


Nitawaonyesha yule munayepaswa kumwogopa; mumwogope Mungu, kwa sababu kisha kuuawa ni yeye anayekuwa na uwezo wa kumutupa mutu katika jehenamu. Hakika ninawaambia, ni huyo munayepaswa kumwogopa!


Wakati ule watu wataanza kuiambia milima ‘Mutuangukie’, navyo vilima ‘Mutufunike!’


Azabu yao itakuwa kuangamizwa kwa milele, na kutengwa mbali na uso wa Bwana na mbali na utukufu wa uwezo wake,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ