Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 19:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Wakati huo, kutakuwa barabara kubwa kutoka inchi ya Misri mpaka katika inchi ya Asuria. Waasuria watawatembelea Wamisri, na Wamisri watawatembelea Waasuria; nao wote watamwabudu Mungu pamoja.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 19:23
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kati ya wale wanaonijua mimi, kuna Wamisri na Wababeli. Vilevile Wafilistini, Watiro na Waetiopia. Wanasema: “Huyu amezaliwa kule.”


Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.


Tena, kutakuwa barabara kubwa toka Asuria kwa ajili ya watu wake waliobaki humo kama ilivyokuwa kwa Waisraeli wakati walipotoka katika inchi ya Misri.


Wakati huo, Israeli itahesabiwa pamoja na Misri na Asuria; mataifa haya matatu yatakuwa baraka kwa dunia yote.


watu wengi wataenda kule na kusema, Mukuje tupandie kwenye mulima wa Yawe, tuende kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo, apate kutufundisha njia zake, nasi tutafuata mapito yake. Maana sheria itakuja kutoka Sayuni; neno la Yawe kutoka Yerusalema.


Siku hiyo, baragumu kubwa itapigwa na watu wote wa Israeli waliopotea katika inchi ya Asuria au waliotawanywa katika inchi ya Misri watarudi na kumwabudu Yawe juu ya mulima mutakatifu kule Yerusalema.


Milima yote nitaifanya kuwa njia, na barabara zangu kubwa nitazitengeneza.


Yawe, Mukombozi na Mutakatifu wa Israeli, anamwambia hivi yule anayezarauliwa sana, yule anayechukiwa na mataifa, na ambaye ni mutumishi wa watawala: Wafalme wataona nao watasimama; wakubwa watainama na kuabudu kwa heshima ya Yawe ambaye anatimiza ahadi zake, kwa heshima ya Mutakatifu wa Israeli ambaye amekuchagua wewe.


Enyi wakaaji wa Yerusalema, mutoke, mutoke inje ya muji, muwatayarishie njia watu wenu wanaorudia! Mujenge! Mujenge barabara na kuondoa mawe yote! Muweke bendera kuwa kitambulisho kwa ajili ya watu.


Katika kila sikukuu ya mwandamo wa mwezi, na katika kila siku ya Sabato, wanadamu wote watakuja kuniabudu. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Siku hiyo wandugu zenu watawarudilia, kutoka Asuria na vijiji vya Misri, kutoka inchi ya Misri na eneo la muto Furati; kutoka sehemu za maji na sehemu za milima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ