Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 19:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mimi nitawachonganisha Wamisri wao kwa wao. Ndugu atapigana na ndugu yake, jirani atapigana na jirani yake, muji mumoja na muji mwingine, mufalme mumoja na mufalme mwingine.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 19:2
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sasa, watu wa Israeli waligawanyika kwa makundi mawili: kundi moja lilimutambua Tibuni mwana wa Ginati kuwa mufalme, na kundi la pili lilimutambua Omuri.


Taifa moja lilipigana na taifa lingine na muji mumoja ulipigana na muji mwingine, kwa sababu Mungu aliwafazaisha kwa taabu za kila aina.


Watu watatesana, kila mutu na mwenzake; vijana watawazarau wazee, na watu wa ovyo ovyo watawazarau wenye heshima.


Mataifa yamesikia jinsi mulivyopata haya, kilio chenu kimeenea katika dunia yote; mashujaa wamegongana wenyewe kwa wenyewe, wote pamoja wameanguka.


Musiregee wala musikuwe na hofu, kwa sababu ya habari munazosikia katika inchi. Mwaka huu kuna habari hii, mwaka mwingine habari ingine; habari ya mateso makali katika inchi, mutawala mumoja anapigana na mutawala mwingine.


Nami nitasababisha kila namna ya kitisho juu ya Gogi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Waaskari wake wataanza kushambuliana wenyewe kwa mapanga yao.


Mbele ya wakati huo, watu hawakupata mushahara kwa kazi zao wala mali kwa ajili ya kutumikisha nyama. Hamukuwa na usalama kwa sababu ya waadui zenu, maana nilisababisha uadui kati ya watu wote.


“Ndugu atamutoa ndugu, kusudi auawe, na baba atamutoa mutoto wake, nao watoto watawageukia wazazi wao na kuwaua.


na adui wa mutu atakuwa wa jamaa yake mwenyewe.


Yesu akitambua mafikiri yao, akawaambia: “Watu wa ufalme wowote wakigombana wao kwa wao, ufalme ule utaanguka. Nao wakaaji wa muji wowote au watu wa jamaa yoyote wakigombana wao kwa wao, muji ule au jamaa ile haitadumu.


Kwa maana taifa litapigana na taifa, na ufalme utapigana na ufalme. Kutakuwa njaa na tetemeko ya inchi katika pahali mbalimbali.


Watu wa ufalme mumoja wakigombana wao kwa wao, ufalme ule utaanguka.


Watu wa Gideoni walipopiga baragumu zao mia tatu, Yawe akawafanya Wamidiani waanze kuuana wao kwa wao katika kambi. Waliobaki wakatoroka mpaka Zerera, wakafika Beti-Sita, hata kwenye mupaka wa Abeli-Mehola karibu na Tabati.


Kisha Mungu akaleta roho ya uadui kati ya Abimeleki na watu wa Sekemu, nao wakamwasi.


Wapelelezi wa Saulo kule Gibea katika inchi ya Benjamina waliwaona watu wengi wakikimbia huku na huko.


Hivyo, Saulo na watu wake wakajipanga na kuingia katika vita na Wafilistini. Lakini Wafilistini walianza kushambuliana wenyewe kwa wenyewe kwa muvurugiko mukubwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ