Isaya 19:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200219 Siku hiyo, kutakuwa mazabahu kwa ajili ya Yawe katikati ya inchi ya Misri, na nguzo iliyotakaswa kwa ajili ya Mungu kwenye mpaka wa Misri. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
lakini tulitaka mazabahu hii ikuwe ushuhuda kati yetu na ninyi na vizazi vyetu vinavyokuja kwamba sisi tuna haki ya kumutumikia Yawe kwa sadaka zetu za kuteketezwa kwa moto na sadaka zetu zingine, na kwa sadaka zetu za amani, kusudi watoto wenu wasipate kuwaambia watoto wetu kwamba hawana fungu lolote lao kwa Yawe.
Tena tulifikiri kwamba ikiwa jambo kama hilo litasemwa juu yetu au juu ya wazao wetu katika siku zinazokuja, tutasema: ‘Muangalie mufano wa mazabahu ya Yawe ambayo wazee wetu waliijenga; sio kwa ajili ya kutolea juu yake sadaka za kuteketezwa kwa moto au sadaka zingine lakini kama ushuhuda kati yetu na ninyi’.