Yawe atakausha guba ya bahari ya Misri, kwa pumzi yake inayochoma atakausha muto Furati, nao utagawanyika katika vijito saba, watu wavuke humo miguu mikavu.
Mungu anasema: Musimike bendera juu ya mulima usiokuwa na miti, muwapigie waaskari kelele, muwapepee watu kwa mukono, mukiwaita waingie kwenye milango ya muji wa wakubwa.
Watu wenu elfu moja watamukimbia askari mumoja adui; na waaskari watano waadui watawakimbiza ninyi wote. Kwa mwisho, watakaobaki, watakuwa kama muti wa bendera kwa mulima, kama kitambulisho kinachokuwa juu ya kilima.
Upanga ukuwe juu ya farasi wake na magari yake, juu ya majeshi yake yote ya mushahara, kusudi wakuwe sawa na wanawake! Upanga ukuwe juu ya hazina zake zote kusudi zinyanganywe.
Waaskari wa Babeli wameshindwa kupigana, wamebaki katika makimbilio yao; nguvu zao zimewaishia, wamekuwa kama wanawake. Nyumba za Babeli zimechomwa kwa moto, milango yake ya chuma imevunjwa.
Watapitia katika bahari ya mateso, nami nitayapiga mawimbi yake, na vilindi vya maji ya muto Nili vitakauka. Kiburi cha Asuria kitavunjwa na nguvu za Misri zitatoweka.
Kweli, nitawashambulia wale waliowakamata mateka, nao watakamatwa mateka na wale waliowafanya watumwa wao. Halafu kwa hiyo mutajua kwamba Yawe wa majeshi ndiye aliyenituma.
Basi, kwa sababu tunajua kwamba ni lazima kumwogopa Bwana, ndiyo maana tunajitoa kuwavuta watu kwake. Mungu anatujua waziwazi nami ninatumaini kwamba ninyi wenyewe munatujua waziwazi vilevile.