Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 18:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Wakati huo, Yawe wa majeshi ataletewa sadaka kutoka kwa watu warefu na wenye ngozi laini, watu wanaotisha kwa karibu na kwa mbali, taifa la watu wenye nguvu na ushindi, ambalo inchi yake imegawanywa na mito. Ataletewa sadaka hizo kwenye mulima Sayuni anapoabudiwa yeye Yawe wa majeshi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 18:7
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wengi sana walikuja wakamuletea Yawe sadaka kule Yerusalema, vilevile wakamuletea Hezekia, mufalme wa Yuda zawadi za bei kali. Hivyo kutoka wakati ule, akasifiwa sana na mataifa mengine yote.


Wajumbe watakuja kutoka Misri, Waetiopia watamuletea Mungu mali zao.


Mupeleke wana-kondoo kwa mutawala wa inchi, mupeleke kutoka Sela katika jangwa mpaka kwenye mulima Sayuni.


Inatuma wajumbe ambao wanasafiri ndani ya muto Nili, wamepanda ndani ya mitumbwi iliyotengenezwa na matete. Muende, enyi wajumbe wepesi, kwa taifa kubwa na hodari, la watu warefu wenye ngozi laini, wanaotisha kwa karibu na kwa mbali, taifa la watu wenye nguvu na ushindi, ambalo inchi yake imegawanywa na mito.


Maana, Yawe ameniambia hivi: Tokea juu kwenye makao yangu nitaangalia yanayotukia, nikitulia kama joto katika mwangaza wa jua, kama wingu la umande wakati wa mavuno.


Yawe anasema hivi: Utajiri wa Misri na faida ya uchuuzi za Kushi, pamoja na za watu wa Seba, wale watu warefu sana, zitakuja kwako mwenyewe wewe taifa la Israeli, zote zitakuwa mali yako. Watu hao watakufuata wakifungwa minyororo; watainama mbele yako na kukusihi wakisema: Kwako kuna Mungu wa kweli, wala hakuna Mungu mwingine lakini yeye.


Yawe anasema: Enyi watu wa Sayuni, musimame muwakanyagekanyage! Nitawapatia nguvu kama ngombe dume mwenye pembe za chuma na kwato za shaba. Mutawasaga watu wa mataifa mengi; mutanitolea mimi mapato yao, mutanitolea mali zao mimi Bwana wa dunia yote.


Wao ni watu wa kuchukiza na kutisha; wao wanajiamulia sheria wenyewe na kujipatia mamlaka.


Kutoka ngambo ya mito ya Kushi watu wangu wanaoniomba, wale ambao wametawanyika, wataniletea sadaka yangu.


Watu wa mataifa katika dunia yote tokea upande jua linapopanda mpaka upande jua linaposhuka wanalitukuza jina langu. Kila pahali wananifukizia ubani na kunitolea sadaka zinazokubaliwa; maana jina langu linatukuzwa kati yao.


Wakaingia ndani ya nyumba, wakamwona mutoto pamoja na mama yake, Maria. Wakapiga magoti na kumwabudu mutoto. Kisha wakafungua mizigo yao na kumutolea zawadi ya zahabu, ubani na marasi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ