Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 18:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Enyi wakaaji wote katika ulimwengu, nanyi munaojaza dunia! Bendera itakaposimikwa kwenye mulima, muangalie! Baragumu itakapopigwa, musikilize.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 18:3
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Zaburi ya Asafu. Mungu, Mungu Yawe, amesema, amewaita wakaaji wa dunia, tokea magaribi mpaka mashariki.


Yawe anasema hivi: Sikiliza enyi mbingu, tega sikio ee dunia. Mimi nimewalea watoto wangu na kuwakomalisha, lakini sasa wameniasi!


Naye atasimika bendera kuwaita mataifa, kuwakusanya Waisraeli waliozarauliwa, kuwaleta pamoja watu wa Yuda waliotawanywa, na kuwarudisha toka pembe ine za dunia.


Mungu anasema: Musimike bendera juu ya mulima usiokuwa na miti, muwapigie waaskari kelele, muwapepee watu kwa mukono, mukiwaita waingie kwenye milango ya muji wa wakubwa.


Musikilize kelele kwenye milima kama za kundi kubwa la watu! Musikilize kelele za falme, na mataifa yanayokusanyika! Yawe wa majeshi analichunguza kundi linalokwenda kwa vita.


Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu, lakini hawauoni. Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya. Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!


Mufalme wao atatoroka kwa ajili ya hofu, na wakubwa wao wataiacha bendera yao kwa ajili ya woga. –Ni ujumbe wa Yawe ambaye moto wake uko katika Sayuni, ambaye furu lake liko katika Yerusalema.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitasimika bendera kwa kuita mataifa; nitayaonyesha kitambulisho. Nayo yatawarudishia wana wenu wakiwabeba kwenye kifua, vilevile na wabinti zenu kwenye mabega.


Yawe ananyunyua bendera kwa kuita taifa la mbali; anawapigia filimbi watu kutoka miisho ya dunia; nao wanakuja mbio na kufika haraka!


Wakati huo, Yawe atawapigia muunzi watu wa Misri wakuje kama mainzi toka vijito vya mito Nili; na watu wa Asuria wakuje kama nyuki kutoka inchi yao.


Ee inchi, ee inchi, ee inchi! Sikia neno la Yawe!


Pandisha bendera ya vita katika dunia, piga baragumu kati ya mataifa; uyatayarishe mataifa kwa kupigana naye; uziite falme kwa kuishambulia; falme za Ararati, Mini na Askenazi. Weka jemadari juu yake; ulete farasi kama makundi ya nzige.


Musikilize enyi watu wote; sikiliza ewe dunia na vyote vinavyokuwa ndani yako. Bwana wetu Yawe anakuja kuwashitaki, Bwana wetu anasema kutoka hekalu lake takatifu.


Musikilize mashitaki ya Yawe, enyi milima, musikilize enyi misingi imara ya dunia! Yawe yuko na maneno juu ya watu wake. Yeye atatoa mashitaki juu ya Waisraeli.


Yawe anawaita wakaaji wa muji, na ni jambo la hekima sana kumutii yeye: Musikilize, enyi watu wa Yuda; musikilize enyi muliokusanyika katika muji.


Yawe atawatokea watu wake; atafyatua mishale yake kama umeme. Bwana wetu Yawe atapiga baragumu; atafika pamoja na upepo mukali wa kusini.


“Lakini heri kwenu, kwa sababu macho yenu yanaona na masikio yenu yanasikia!


Basi mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ