Isaya 17:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
5 Itakuwa kama wakati wa mavuno, wakati wamekwisha kuokota ngano, na kukusanya masuke katika mukono. Hakika, itakuwa kama bonde la Refaimu wakati wamekwisha kuvuna ngano.
hata mukiifanya ikomae siku hiyohiyo muliyoipanda na kuifanya ichanue asubui hiyohiyo, mavuno yenu yatatoweka siku hiyo ya hasara na maumivu yasiyoweza kuponyeshwa.
Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Babeli ni kama uwanja wa kupepetea ngano wakati unapotayarishwa. Lakini bado kidogo tu, wakati wa mavuno utaufikia.
Muviache vyote viwili vikomae pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati ule nitawaambia wavunaji: muongoe kwanza nyasi, nanyi muzilundike kwa mafungu mafungu kwa kuzichoma, na kisha mukusanye ngano na kuweka mavuno ndani ya gala yangu.’ ”
Kisha, mupaka huo ulipitia kwenye Bonde la Hinomu, upande wa kusini wa kilima cha Wayebusi, ni kusema Yerusalema, kuelekea kilele cha mulima unaokuwa upande wa magaribi wa bonde la Hinomu na kufika mwisho wa bonde la Refaimu.
Kisha ulielekea chini kupitia pembeni ya mulima unaokuwa karibu na bonde la mwana wa Hinomu, ambalo lilikuwa katika sehemu ya kaskazini zaidi ya bonde la Warefaimu. Halafu mupaka uliteremuka kuelekea bonde la Hinomu, upande wa kusini wa kilima cha Wayebusi, ukaendelea kuteremuka mpaka Eni-Rogeli.