Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 17:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Wakati wa magaribi yanaleta hofu kubwa, lakini mbele ya asubui yametoweka! Ndilo litakalowapata wale wanaotukamata na kutunyanganya mali yetu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 17:14
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nao wakamwambia Isaya: “Hezekia anasema hivi: ‘Leo ni siku ya huzuni, ya kuazibiwa na ya kuzarauliwa. Sisi tumekuwa kama mwanamuke anayetaka kuzaa mutoto, lakini hana nguvu ya kumuzaa.


Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.


Hii ndiyo sehemu ya mutu mwovu kutoka kwa Mungu, ndio mwisho aliopangiwa na Mungu.


Kisha nikapita pale, naye hakukuwa tena; nikamutafuta, lakini hakuonekana tena.


Maana Yawe atawatetea; atagandamiza maisha ya wale wanaowagandamiza.


Maana bado kidogo, nayo hasira yangu itapita na kasirani yangu itawageukia Waasuria.


Nami mulinzi nikajibu: Asubui inakuja, vilevile usiku; ukitaka kuuliza, uliza tu; kwenda urudi tena.


lakini mimi Mungu nitahuzunisha Yerusalema, ndani yake kutakuwa vilio na maombolezo, muji wenyewe utakuwa kama mazabahu.


Kundi la waadui zako litakuwa kama mavumbi laini, waliokutendea ukali watakuwa kama maganda. Hayo yatafanyika kwa rafla.


Halafu, kundi la mataifa yote yanayoshambulia Yerusalema, wote wanaoshambulia ukuta wake na kuutia wasiwasi, watatoweka kama ndoto, kama maono ya usiku.


Pumzi yake ni kama mafuriko ya muto ambao maji yake yanafika mpaka kwenye shingo. Anakuja kupepeta mataifa kwa lungo ya maangamizi, kuwafunga lijamu na kuwapeleka wasikotaka.


Ole kwako! Unaangamiza ingawa hauangamizwi. Unadanganya ingawa haudanganywi. Utakapokwisha kuangamiza, wewe utaangamizwa! Utakapomaliza kudanganya, wewe utadanganywa.


Mutakumbuka kitisho kilichopita na kujiuliza: Wako wapi wale waliokadirisha na kuchunguza kodi? Wako wapi wale waliopeleleza ugumu wa kuta zetu?


Yawe amepanga sehemu ya kila mumoja wao, ametumia kamba kuwapimia inchi hiyo; watairizi milele na milele, wataishi mule kizazi hata kizazi.


Utawatafuta hao wanaopingana nawe, hautawaona tena; wale wanaofanya vita nawe, watakuwa wameangamia.


Yawe anasema: Hayo ndiyo yatakayokupata, ni hivi nilivyoamua kukutendea, kwa sababu umenisahau mimi na kutegemea miungu ya uongo. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Israeli, ulikuwa wangu wa pekee, kama malimbuko ya shamba langu. Wote waliokukula walibeba hukumu, wakipatwa na hasara. –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini nimemunyanganya Esau kila kitu, nimeyafunua maficho yake, wala hawezi kujificha tena. Watoto, wandugu na jirani zake wameangamizwa; hakuna hata mumoja aliyebaki.


Hawatahitaji kuokota kuni katika mashamba, wala kukata miti katika pori, kwa sababu watazitumia hizo silaha kwa kuwasha nazo moto. Watabeba mali za wale walioteka mali zao na kuwanyanganya mali zao. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Yawe wa majeshi, ambaye kwa utukufu wake amenituma, anasema hivi juu ya mataifa yaliyowakamata mateka watu wake: Hakika, anayewagusa ninyi anagusa mboni ya jicho langu.


“Ee Yawe, waangamie waadui zako wote! Lakini warafiki zako wakuwe kama jua, wakati linapochomoza kwa mwangaza mukubwa!” Inchi ya Waisraeli ikakuwa na amani kwa muda wa miaka makumi ine.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ