Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 17:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Mataifa yananguruma kama ngurumo ya maji mengi, lakini Mungu atayakaripia, nayo yatakimbilia mbali. Yatafukuzwa kama maganda juu ya mulima mbele ya upepo; kama mavumbi yanayonyanyuliwa na upepo mukali.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 17:13
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, wapeperushwe kama majani yenye kukauka, wakuwe kama maganda yanayopelekwa na zoruba!


na kuiambia: “Mwisho wako ni hapa, si zaidi! Mawimbi yako ya nguvu yatakomea hapa!”


Lakini waovu si vile hata kidogo. Wao ni kama maganda yanayopeperushwa na upepo.


Wakuwe kama maganda yanayopeperushwa na upepo, wakikimbizwa na malaika wa Yawe!


Kwa nguvu yako uliisimika milima pahali pake. Wewe una nguvu nyingi!


Unatuliza uvumi wa bahari na wa mawimbi yake, unakomesha fujo za watu.


Umeitetea haki yangu katika maneno yangu; umeikaa katika kiti chako cha kifalme, wewe mwamuzi wa haki.


Nitauvunja uwezo wa Waasuria katika inchi yangu; nitawakanyagakanyaga katika milima yangu. Nitawaondolea watu wangu nira yao ya unyanganyi, na muzigo wa mateso yao.


Maana wamekimbia mapanga, mapanga yaliyochomolewa, pinde zilizovutwa na ukali wa mapigano.


na kukuzungushazungusha, kisha atakutupa kama mupira mpaka katika inchi pana. Huko utakufia karibu na magari yako ya vita unayojivunia, wewe unayezaraulisha nyumba ya bwana wako.


Siku hiyo, Yawe atakamata upanga wake mukubwa, mukali na imara, na kuiazibu Leviatani, ile nyoka inayoruka na kuzongazonga. Yawe ataua nyoka mukubwa anayeishi katika bahari.


Kundi la waadui zako litakuwa kama mavumbi laini, waliokutendea ukali watakuwa kama maganda. Hayo yatafanyika kwa rafla.


Pumzi yake ni kama mafuriko ya muto ambao maji yake yanafika mpaka kwenye shingo. Anakuja kupepeta mataifa kwa lungo ya maangamizi, kuwafunga lijamu na kuwapeleka wasikotaka.


Yawe amepanga sehemu ya kila mumoja wao, ametumia kamba kuwapimia inchi hiyo; watairizi milele na milele, wataishi mule kizazi hata kizazi.


Kwake mataifa ni kama tone la maji katika mbeketi, ni kama mavumbi juu ya kilo. Kwake visanga ni vyepesi kama mavumbi laini.


Mara tu wanaposimikwa na kuanza kuota, hata mbele hawajatoa mizizi kama miti katika udongo, Yawe akiwapulizia wananyauka, upepo mukali unawapeperusha kama makapi!


Kweli! Wote waliokukasirikia, watapata haya na kufezeheka. Wote wanaopingana nawe, watakuwa wa bure na kuangamia.


basi, Bwana wao atawaletea mafuriko makubwa ya maji ya muto Furati, ni kusema mufalme wa Asuria na nguvu zake zote; yatafurika na kupita kingo zake.


Mara moja chuma, udongo wa mufinyanzi, shaba, feza na zahabu, vyote vikavunjika vipandevipande na vikakuwa kama maganda kwenye nafasi ya kupepetea ngano wakati wa jua. Upepo ukavipeperushia mbali wala hakukubakia hata kipande kimoja. Lakini lile jiwe lililoivunja ile sanamu likageuka kuwa mulima mukubwa na kuijaza dunia yote.


Basi, watatoweka kama ukungu wa asubui, kama umande unaotoweka upesi; kama makapi yanayopeperushwa kwenye nafasi ya kupepetea, kama moshi unaotoka katika munara wa kutoshea moshi inje.


mbele hamujapeperushwa mbali kama maganda, mbele haijawafikia siku ya hasira kali ya Yawe, mbele haijawafikia siku ya kasirani ya Yawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ