Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 17:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ujumbe wa Mungu juu ya muji wa Damasiki. Damasiki utakoma kuwa muji; utakuwa lundo la mabomoko.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 17:1
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kule, akagawanya jeshi lake katika makundi. Usiku, akawashambulia waadui zake, akawashinda na kuwafukuza mpaka Hoba, upande wa kaskazini wa Damasiki.


Lakini Abramu akasema: “Ee Yawe, utanipa nini wakati ninaendelea kuishi bila mutoto, na murizi wangu ni Eliezeri wa Damasiki?


Nyuma ya Daudi kufanya mauaji kule Zoba, Resoni alikusanya watu, naye mwenyewe akakuwa kiongozi wao. Basi, wakaenda Damasiki, wakakaa kule na kumufanya Resoni mufalme wa Damasiki.


Tigilati-Pileseri, akiitika kwa ombi la Ahazi, aliushambulia muji wa Damasiki na kuuteka. Akamwua mufalme Resini na kuwapeleka wafungwa kule Kiri.


Nao Waaramu wa Damasiki, walipokwenda kumusaidia Hadadezeri mufalme wa Zoba, Daudi akawashambulia na kuwaua watu elfu makumi mbili na mbili.


Kwa sababu alitolea sadaka kwa miungu ya Damasiki iliyokuwa imemushinda katika vita akisema: “Kwa sababu miungu ya Suria iliwasaidia wafalme wa Shamu, nikiitolea sadaka labda itanisaidia nami vilevile.” Lakini ilisababisha kuangamia kwake na taifa lote la Israeli.


Yawe, Mungu wake akamwacha mufalme Ahazi ashindwe na mufalme wa Suria ambaye vilevile akawapeleka watu wake wengi, akarudi nao Damasiki. Vilevile, alimufanya ashindwe na mufalme wa Israeli ambaye alimushinda na kuua watu wengi sana.


Si kweli kwamba muji wa Kalno niliutendea kama vile wa Karkemisi, muji wa Hamati kama muji wa Arpadi, Samaria kama Damasiki?


Haya ni maono, ambayo nabii Isaya mwana wa Amozi, aliyofunuliwa na Mungu juu ya inchi ya Babeli:


Ujumbe wa Mungu juu ya inchi ya Moabu. Muji wa Ari katika inchi ya Moabu umeangamizwa usiku; muji wa Kiri katika inchi ya Moabu umeangamizwa usiku.


Ujumbe wa Mungu juu ya inchi ya Misri. Yawe amepanda juu ya wingu linaloenda mbio na kuja mpaka katika inchi ya Misri. Sanamu za miungu ya Wamisri zitatetemeka mbele yake, mioyo ya Wamisri itayeyuka kwa woga.


Umeufanya muji kuwa lundo la mawe, muji wenye pango kuwa uharibifu. Nyumba za watu wageni zimetoweka, wala hazitajengwa tena upya.


Haujasikia, ewe Saniharibu, kwamba mimi Yawe nilipanga jambo hili tangu zamani? Ninachotimiza sasa nilikipanga zamani. Nilikuweka uifanye miji yenye kuzungukwa na kuta kuwa lundo la mabomoko.


Maana, mbele mutoto huyo hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, inchi za wafalme hao wawili unaowaogopa zitakuwa ukiwa.


Maana muji mukubwa wa Aramu ni Damasiki, na huyo Resini ni mukubwa wa Damasiki tu. Muji mukubwa wa Efuraimu ni Samaria, na mwana wa Remalia ni mukubwa wa Samaria tu. Katika miaka makumi sita na mitano utawala wa Efuraimu utavunjwa; Efuraimu halitakuwa taifa tena. Kama hautaamini, hautaimarika.


Maana mbele mutoto huyu hajafikia umri wa kuweza kutamka neno “Baba” au “Mama”, utajiri wa muji wa Damasiki na vitu walivyonyanganya kule Samaria vitapelekwa kwa mufalme wa Asuria.


Kwa hiyo, siku zinakuja ambapo nitavumisha sauti ya vita juu ya Raba muji wa Waamoni. –Ni ujumbe wa Yawe.– Raba utakuwa lundo la uharibifu, vijiji vyake vitateketezwa kwa moto. Halafu Israeli atatwaa tena urizi wake. Ni Yawe anayesema hivyo.


Kwa hiyo, anasema hivi: Muji wa Samaria nitaufanya kuwa mabomoko katika mbuga, shamba ambalo watu watapanda mizabibu. Mawe yaliyoujenga nitayatupa ndani ya bonde, na misingi yake nitaichimbuachimbua.


Basi! Kwa sababu yenu, Sayuni utalimwa kama shamba, Yerusalema lundo la makokoto, nao mulima wa hekalu utakuwa pori.


Ujumbe wa Yawe: Neno la Yawe ni juu ya azabu ya miji Hadiraki na Damasiki. Maana inchi ya Aramu ni mali ya Yawe, kama vile makabila yote ya Israeli yanavyokuwa,


na kumwomba amwandikie barua za kumutambulisha katika nyumba za kuabudia za muji Damasiki. Katika barua hizo, Saulo alipewa ruhusa kwamba akiona watu wanaofuata Njia ya Bwana, ikiwa wanaume au wanawake, awafunge na kuwapeleka Yerusalema.


hakika mutawaua kwa upanga watu wa muji huo. Mutauteketeza kwa upanga kabisa na ngombe wote vilevile.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ