Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 16:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Wakimbizi wa Moabu waishi kwenu, mukuwe kimbilio lao mbali na mwangamizaji. Mutesaji atakapokuwa ametoweka, mateso yatakapokuwa yamekoma, na wagandamizaji kutoweka katika inchi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 16:4
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

utaimba wimbo huu wa kumuchekelea mufalme wa Babeli: Jinsi gani mutesaji alikomeshwa! Ukali wake umekomeshwa!


Kijito cha Nimurimu kimekauka; nyasi zimekauka, majani mabichi yamenyauka, hakuna chochote kinachoota hapo.


Yawe ataulinda mulima wa Sayuni, lakini watu wa Moabu watakanyagwakanyagwa ndani ya inchi yao kama nyasi katika shimo la mboleo.


Ole kwako! Unaangamiza ingawa hauangamizwi. Unadanganya ingawa haudanganywi. Utakapokwisha kuangamiza, wewe utaangamizwa! Utakapomaliza kudanganya, wewe utadanganywa.


Nitawasukuma watesaji wako wakule miili yao wenyewe; watalewa damu yao wenyewe kama divai. Halafu wanadamu wote watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mwokozi wako, Mukombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.


Wewe umenisahau mimi Yawe Muumba wako, niliyezitandaza mbingu, na kuiweka misingi ya dunia! Kwa sababu ya kasirani ya yule anayekutesa, unaendelea kuogopa siku zote kwamba yuko tayari kukuangamiza! Lakini hasira yake itafikia wapi?


Utaimarishwa katika haki, mbali na kaoneo, nawe hautaogopa kitu; mbali na hofu, maana haitakukaribia.


Mafungo ya kweli ni kugawanya chakula chako pamoja na wenye njaa, kuwakaribisha katika nyumba yako wamasikini wasiokuwa na makao, kuwavalisha wasiokuwa na nguo, bila kusahau kuwasaidia wandugu zenu.


Viatu vyote vya washambulizi katika vita na nguo zote zenye kujaa damu vitateketezwa kama kuni za kuwasha moto.


Enyi jamaa ya Daudi, Yawe anasema hivi: Kila asubui muamue maneno kufuatana na sheria yangu, muwakomboe wote walionyanganywa mali zao toka katika mikono ya watesaji. Kama si vile, hasira yangu itawaka kama moto, wala hakuna atakayeweza kuizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.


Vilevile Wayuda waliokuwa katika inchi ya Moabu na kati ya Waamoni na katika inchi ya Edomu na inchi zingine, waliposikia kwamba mufalme wa Babeli amewaruhusu Wayuda wengine kubaki katika inchi ya Yuda na kwamba amemusimika Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu kuwa mutawala wao,


Enyi wenyeji wa Diboni: mushuke kutoka pahali penu pa utukufu, muikae juu ya udongo usiokuwa na maji. Maana mwangamizaji wa Moabu, amefika kuwashambulia; amekwisha haribu kuta zenu.


Mwangamizaji atapita katika kila muji, hakuna muji utakaomwepuka; mabonde yataangamia, nafasi zenye kunyooka zitaharibiwa, kama vile Yawe alivyosema.


hamukupaswa kusimama kwenye masanganjia na kuwakamata wakimbizi wao, hamukupaswa kuwatoa kwa waadui zao wale waliobaki wazima.


Watu wa Yuda watakuwa kama mashujaa katika vita, watawakanyaga waadui zao ndani ya matope katika njia. Watapigana kwa sababu mimi Yawe nipo pamoja nao; nao watawafezehesha hata waaskari wapanda-farasi.


Mimi mwenyewe nitailinda inchi yangu, nitazuia majeshi yasipitepite ndani. Hakuna mutu atakayewatesa tena watu wangu, maana, kwa macho yangu mwenyewe, nimeona jinsi walivyoteseka.


Wamoja watauawa kwa vita na watapelekwa kuwa wafungwa katika inchi za mataifa yote. Vilevile mataifa mengine yatautawala Yerusalema mpaka nyakati zao za kuutawala zitakapokwisha.”


Mungu, anayeleta amani, atamupondaponda sasa hivi Shetani chini ya miguu yenu. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo ikuwe pamoja nanyi.


“Usimutese mutumishi wako wa mushahara anayekuwa masikini na muhitaji, akuwe Mwisraeli au mumoja wa wageni wanaoishi katika miji yenu.


Lakini uache kiwanja kinachokuwa inje ya hekalu, usikipime kwa maana kimetolewa kwa watu wa mataifa mengine watakaokanyaga muji mutakatifu kwa muda wa miezi makumi ine na miwili.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ