Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 16:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Wamoabu wanawaambia watu wa Yuda: Mutuongoze, mutuamue. Mueneze ulinzi wenu juu yetu, kama vile usiku unavyoeneza kivuli chake. Mutufiche sisi wakimbizi; musitutoe sisi tuliofukuzwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 16:3
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

na wakati Yezebeli alipowaua manabii wa Yawe, Obadia aliwachukua manabii mia moja, akawaficha makumi tano tano ndani ya pango, akakuwa anawapelekea chakula na maji.


mujifunze kutenda mema. Mufuate sheria ya Mungu, mumusaidie mwenye kuteswa, mumupatie yatima haki yake, mutetee haki za wajane.


Maana wewe umekuwa kimbilio kwa wazaifu, pango kwa wakosefu katika taabu zao. Wewe ni kimbilio wakati wa zoruba, kivuli wakati wa joto kali. Kweli pigo la watu wakali ni kali kama zoruba inayopiga ukuta;


Kila mumoja atakuwa kama pahali pa kujikinga na upepo, kama pahali pa kujificha wakati wa mvua kubwa. Watakuwa kama vijito vya maji katika inchi yenye kukauka, kama kivuli cha jiwe kubwa katika jangwa.


–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe, yule anayewakusanya Waisraeli waliosambazwa.– Zaidi ya hao niliokwisha kukusanya, nitawakusanya watu wengine wakutane nao.


Mafungo ya kweli ni kugawanya chakula chako pamoja na wenye njaa, kuwakaribisha katika nyumba yako wamasikini wasiokuwa na makao, kuwavalisha wasiokuwa na nguo, bila kusahau kuwasaidia wandugu zenu.


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Enyi jamaa ya Daudi, Yawe anasema hivi: Kila asubui muamue maneno kufuatana na sheria yangu, muwakomboe wote walionyanganywa mali zao toka katika mikono ya watesaji. Kama si vile, hasira yangu itawaka kama moto, wala hakuna atakayeweza kuizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.


Yawe anasema hivi: Mufuate sheria yangu na kutenda kwa haki. Muokoe kila mutu aliyenyanganywa mali zake toka katika mikono ya mutesaji. Musiwatendee vibaya au kwa ukali wageni, wayatima na wajane, wala musimwange damu ya mutu asiyekuwa na kosa kwa nafasi hii.


Basi, akasema kwa sauti: Angalia Babeli, muji mukubwa nilioujenga kwa nguvu zangu ukuwe makao yangu ya kifalme na kwa ajili ya utukufu wangu!


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mutoe hukumu kwa haki, mutende mema na kuwa na huruma ninyi kwa ninyi.


Kwa maana nilisikia njaa, mukanipa chakula; nilisikia kiu, mukanipa maji; nilikuwa mugeni, mukanikaribisha;


Musisahau kuwakaribisha wageni, maana kwa kufanya hivi wamoja wamewakaribisha wamalaika pasipo kujua.


Muti wa miiba ukajibu: ‘Kama kweli munataka kunichagua kuwa mufalme, mukuje mukae chini ya kivuli changu. Lakini kama hamutaki kufanya hivyo, basi moto utoke kwenye miiba yangu na kuiteketeza hata mierezi ya Lebanoni.’ ”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ