Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 16:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Lakini sasa Yawe anasema hivi: Nyuma ya miaka mitatu kamili, ikihesabiwa kama vile mutumishi anavyohesabu siku zake, utukufu wa Moabu utapunguka. Ingawa watu wake ni wengi, watakaobaki wazima watakuwa wachache na wazaifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 16:14
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yakobo akasikia kwamba wana wa Labani walinungunika na kusema: “Yakobo amepeleka kila kitu cha baba yetu; ndivyo alivyopata kuwa tajiri.”


Halafu akaanza kueleza juu ya utajiri anaokuwa nao, wana anaokuwa nao, jinsi mufalme alivyomupandisha cheo, na jinsi alivyopewa madaraka zaidi kuliko wakubwa wengine wote wa mufalme.


Angalia pembeni basi, umwache, kusudi apate kufurahia siku zake kama mutumishi wa mushahara.


Mwanadamu ana magumu katika dunia, na siku zake ni kama siku za mutumishi wa mushahara!


Wote pamoja watashambulia Wafilistini wanaokuwa upande wa magaribi, pamoja watawanyanganya watu wanaokaa upande wa mashariki. Watawashinda Waedomu na Wamoabu, nao Waamoni watawatii.


Moyo wangu unaugua kwa ajili ya inchi ya Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Zoari, wanakimbia mpaka Egilati-Selisiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhiti wakilia, katika njia kwenda Horonaimu wanatoa kilio cha maangamizi.


Hili ndilo jambo Yawe alilosema wakati uliopita juu ya Moabu.


Siku hiyo, utukufu wa Yakobo utaporomoshwa, na unono wake utapotea.


Maana Bwana aliniambia hivi: Katika muda wa mwaka mumoja, bila kuzidi wala kupunguka, utukufu wote wa Kedari utakwisha.


Ni Yawe wa majeshi! Yeye ndiye aliyeyapanga haya yote. Alifanya hivyo akiharibu kiburi chao na kuwapatisha haya waheshimiwa wake.


Yawe ataulinda mulima wa Sayuni, lakini watu wa Moabu watakanyagwakanyagwa ndani ya inchi yao kama nyasi katika shimo la mboleo.


Watainyoosha mikono yao kama mutu anayejaribu kuogelea, lakini pamoja na bidii yao, Yawe ataporomosha kiburi chao.


Maana, mbele mutoto huyo hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, inchi za wafalme hao wawili unaowaogopa zitakuwa ukiwa.


Wamoabu wataangamizwa, hata hawatakuwa tena taifa, kwa sababu walijitukuza mbele ya Yawe.


Anayetaka kujivuna, ajivune kwamba ananifahamu mimi, kwamba anajua kwamba mimi Yawe ninatenda mema, ninafanya mambo ya haki kufuatana na sheria yangu katika dunia. Watu wa namna hiyo ndio wanaonipendeza. –Ni ujumbe wa Yawe.


Pahali pake, mufungue mikono yenu na kumukopesha kwa mapenzi kiasi cha kutosha mahitaji yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ