Isaya 14:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
8 Miti ya shindano inafurahia kuanguka kwako, nayo mierezi ya Lebanoni pamoja inasema: Kwa vile sasa umeangushwa, hakuna mukata miti atakayekuja juu yetu!
Umewatuma watumishi wako kumuchekelea Bwana wenu; wewe umesema: Kwa magari yangu mengi ya vita, nimefika juu kwenye vichwa vya milima, mpaka kwenye vichwa vya milima ya Lebanoni. Nimeangusha mierezi yake mirefu, na misunobari mizurimizuri. Nimevifikia vichwa vyake na ndani ya pori zake kubwa.
Niliyafanya mataifa yatetemeke kwa sauti ya kuanguka kwake, wakati nilipouangusha chini katika kuzimu pamoja na wale wanaoshuka ndani ya shimo kwa wafu. Nayo miti yote ya Edeni, miti mizuri na ya pekee ya Lebanoni ambayo ilimwangiliwa maji, ilifarijiwa huko chini kwa wafu.
Muomboleze, enyi misunobari, kwa sababu mierezi imeteketea. Miti hiyo mitukufu imeharibiwa! Enyi mialo ya Basani, muomboleze, kwa maana pori kubwa limekatwa!