Kwa hiyo, Yawe alimuleta mufalme wa Wakaldea ambaye aliwaangamiza vijana wao kwa upanga hata ndani ya Pahali Patakatifu; wala hakumuhurumia mutu yeyote akuwe kijana au binti, muzee au muzaifu. Wote Yawe aliwatia katika mikono yake.
Kama mutu anayenyoosha mukono kwenye chicha, ndivyo nilivyokamata mali ya mataifa; kama mutu anayeokota mayai yaliyoachwa ndani ya chicha, ndivyo nilivyoyaokota katika dunia yote. Watu wote walikuwa sawa ndege ambaye hapigi mabawa au kufungua midomo kwa kupiga kelele. Lakini Yawe anasema hivi:
wafalme wote wa kaskazini, wanaokuwa mbali na karibu, mumoja kisha mwingine. Hivi nikakunywesha falme zote za ulimwengu. Na kwa mwisho naye mufalme wa Babeli akakunywa.
basi, nitayaita makabila yote ya kaskazini pamoja na mutumishi wangu Nebukadneza, mufalme wa Babeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitawaleta waishambulie inchi hii na wakaaji wake pamoja na mataifa yote jirani. Nitawaangamiza kabisa, na kuwafanya kuwa kitu cha kuchukiza, cha kuzomewa na kuzarauliwa milele.
Mimi, ninapigana nawe, ewe mwenye kiburi. –Ni ujumbe wa Bwana wa wote, Yawe wa majeshi.– Maana siku yako ya azabu imefika, wakati nitakapokuazibu umetimia.
Sikiliza ninavyolalamika; hakuna wa kunifariji. Waadui zangu wote wamesikia juu ya taabu yangu: wanafurahi kwamba umeniletea hasara. Uifanye ile siku uliyoahidi ifike, uwafanye nao wateseke kama mimi.
Zaidi ya hayo, divai inapotosha; mutu mwenye kiburi hatadumu. Yuko tayari kuwameza wengine kama kuzimu; kama vile kifo, hatosheki na kitu. Anajikusanyia mataifa yote, na watu wote kama mali yake.