Wakimbizi wa Moabu waishi kwenu, mukuwe kimbilio lao mbali na mwangamizaji. Mutesaji atakapokuwa ametoweka, mateso yatakapokuwa yamekoma, na wagandamizaji kutoweka katika inchi.
Nimeonyeshwa maono ya kutisha: wadanganyifu wanadanganya na waangamizaji wanaangamiza. Mupande kwa kupigana vita, enyi Waelamu! Mushambulie, enyi Wamedi! Mungu atakomesha mateso yote yaliyoletwa na Babeli.
Nitawasukuma watesaji wako wakule miili yao wenyewe; watalewa damu yao wenyewe kama divai. Halafu wanadamu wote watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mwokozi wako, Mukombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.
Wewe umenisahau mimi Yawe Muumba wako, niliyezitandaza mbingu, na kuiweka misingi ya dunia! Kwa sababu ya kasirani ya yule anayekutesa, unaendelea kuogopa siku zote kwamba yuko tayari kukuangamiza! Lakini hasira yake itafikia wapi?
Nami nitakitia katika mikono ya wanaokutesa, waliokuambia ulalie tumbo wapite juu yako, nawe ukaufanya mugongo wako kama vile udongo wa njia, kama vile barabara ya kupitia.
Nitawafanya kuwa kitu cha kuchukiza mbele ya falme zote za dunia. Watakuwa kitu cha zihaka, kitu cha kuzomewa, kuchekelewa na kulaaniwa kila fasi nitakapowasambaza.
Utakuwa kitu cha kuzarauliwa na cha haya, mufano wa kitu cha kuchukiza kwa makabila yanayokuzunguka, wakati nitakapotimiza hukumu zangu juu yako kwa hasira na kasirani yangu kali. Ni mimi Yawe ninayasema hivyo.
Mateso uliyoyatenda kule Lebanoni yatakulemea wewe; uliwaua nyama, nyama nao watakuogopesha. Yote hayo yatakupata wewe, kwa mauaji na mateso uliyoitendea dunia, uliyoifanyia miji na wakaaji wake wote.
Nikaona kwamba yule mwanamuke amelewa kwa damu ya watu wa Mungu na ya watu waliouawa kwa sababu ya ushuhuda wao kwa ajili ya Yesu. Wakati nilipomwona nikashangaa sana.
wakisema: “Ole! Ole kwa muji ule mukubwa. Ulikuwa unavaa nguo zilizofumwa na nyuzi nzuri pamoja na nguo zuri ya rangi nyekundu nyeusi na nyekundu sana. Ulikuwa unapambwa kwa zahabu, mawe ya bei kali, na ushanga wa bei kali!
Enyi mbingu, nanyi watu wa Mungu pamoja na mitume na manabii wake, mufurahi kwa ajili ya mambo yaliyotokea muji ule, kwa maana Mungu amewapatia haki yenu kwa kuuhukumu!