alimutuma mwana wake Yoramu kwa mufalme Daudi kwa kumupelekea salamu na shukrani kwa sababu alikuwa amepigana na Hadadezeri na kumushinda. Maana Hadadezeri alipigana na Toi mara nyingi. Yoramu alimupelekea Daudi zawadi za vyombo vya feza, zahabu na shaba.
Maana wewe umekuwa kimbilio kwa wazaifu, pango kwa wakosefu katika taabu zao. Wewe ni kimbilio wakati wa zoruba, kivuli wakati wa joto kali. Kweli pigo la watu wakali ni kali kama zoruba inayopiga ukuta;
Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninaweka katika Sayuni jiwe la musingi, jiwe ambalo limeimarishwa. Jiwe la pembe, la bei kali, jiwe ambalo ni la musingi imara; jiwe linalokuwa na maandiko haya: Anayeamini hataanguka.
Maana kutakuwa watu watakaobaki kule Yerusalema; kule kwenye mulima Sayuni kutakuwa watu wachache watakaobakia. Yawe wa majeshi amekusudia kukamilisha hayo.
Wakati huo, mufalme Merodaki-Baladani mwana wa Baladani, mufalme wa Babeli, aliposikia kwamba Hezekia alikuwa mugonjwa na sasa amepona, alimutumia wajumbe waliomupelekea barua pamoja na zawadi.
Ndimi ninasema juu ya mufalme Kiro: Ni muchungaji niliyemuchagua kwa ajili yangu. Yeye atatimiza mipango yangu yote. Ndimi ninayesema juu ya Yerusalema: Wewe Yerusalema utajengwa tena upya; na juu ya hekalu: Musingi wako utawekwa tena.
Mutakapolia kwa kuomba musaada, basi ile lundo ya sanamu zenu iwaokoe! Upepo utavipeperushia mbali; pumzi itavitupilia mbali. Lakini watakaotafuta kimbilio kwangu, watarizi inchi, mulima wangu mutakatifu utakuwa mali yao.
Basi, nikakuwa muchungaji wa kondoo ambao wachuuzi waliwatayarisha kwenda kuchinjwa. Nikatwaa fimbo mbili: moja nikaiita “Rehema”, na ingine nikaiita “Umoja”, nikaenda kuchunga kondoo.
Lakini ninyi mumefikia kwenye mulima Sayuni na kwenye muji wa Mungu Mwenye Uzima, ndio muji Yerusalema wa mbinguni, kunakokuwa maelfu na maelfu ya wamalaika.
Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.