Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 14:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ewe Israeli, wakati Yawe atakapokufariji nyuma ya mateso, mahangaiko na utumwa uliofanyiwa,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 14:3
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa kitambulisho kwa mataifa; mataifa yatamutafuta na makao yake yatatukuka.


Siku hiyo mutasema: Ninakushukuru, ee Yawe, maana ingawa ulinikasirikia, hasira yako imetoweka, nawe umenifariji.


Watu wangu watakaa katika makao ya amani, katika pahali penye usalama na nafasi yenye utulivu.


Museme na watu wa Yerusalema kwa upole, muwaambie kwamba utumwa wao umekwisha, wamesamehewa uovu wao. Yawe amewaazibu mara mbili kwa sababu ya zambi zao zote.


Itawabidi kuiacha hiyo inchi yenu niliyowapa, nami nitawafanya muwatumikie waadui zenu katika inchi musiyoijua, kwa sababu hasira yangu imewaka kama moto usiozimika hata milele.


Usiogope ee Yakobo, mutumishi wangu, wala usifazaike, ee Israeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Maana nitakuokoa toka huko mbali unapokuwa, nitawaokoa wazao wako kutoka katika uhamisho. Utarudi na kuishi kwa amani, wala hakuna mutu atakayekuogopesha.


Siku hiyo itakapofika, nitaivunja nira inayofungiwa katika shingo lao na kukata minyororo yao.


Lakini mimi, Mukombozi wao ni mwenye nguvu. Yawe wa majeshi ndilo jina langu. Hakika nitatetea maneno yao kusudi nilete amani katika inchi yao, lakini taabu kwa wakaaji wa Babeli.


Mungu anasema: Mataifa jirani za Waisraeli ambayo yalikuwa yanawauzi hayataweza tena kuwaumiza Waisraeli kama vile kwa miiba na michongoma. Halafu watajua kwamba mimi ni Bwana wao Yawe.


Ninachomwa na upendo mukubwa kwa ajili ya Sayuni, na ninawaka kasirani nyingi juu ya waadui zake.


na kuwafanya wakae katika Yerusalema. Wao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; nitatawala juu yao kwa uaminifu na haki.


Kwa hiyo mutawatumikia waadui zenu ambao Yawe atawatuma mbele yenu, kwa njaa, kiu na uchi, na ukosefu wa kila kitu. Atawafunga nira ya chuma mpaka awaangamize.


Enyi mbingu, nanyi watu wa Mungu pamoja na mitume na manabii wake, mufurahi kwa ajili ya mambo yaliyotokea muji ule, kwa maana Mungu amewapatia haki yenu kwa kuuhukumu!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ