Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 14:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Musishangilie, enyi Wafilistini wote, kwamba Asuria, fimbo iliyowapiga, imevunjika; maana, nyoka wa kawaida atazaa nyoka mwenye sumu, na nyoka mwenye sumu atazaa nyoka mukubwa mwenye kuruka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 14:29
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Aliwapiga Wafilistini mpaka muji wa Gaza na inchi iliyouzunguka, kuanzia kwenye munara wa walinzi mpaka muji wenye kuta.


Uzia akaondoka kwa kupigana vita na Wafilistini, akabomoa kuta za miji ya Gati, Yabune na Asidodi. Akajenga miji katika eneo la Asidodi na fasi ingine katika inchi ya Filistia.


Wakati uleule, Wafilistini walikuwa wakiishambulia miji ya Sefela na Negebu ya Yuda. Walinyanganya miji ya Beti-Semesi, Ayaloni, Gederoti, Soko na vijiji vyake, Timuna na vijiji vyake, Gimuzo na vijiji vyake, wakafanya makao yao kule.


Usishangilie kuanguka kwa adui yako; usifurahie ndani ya moyo wako kujikwaa kwake,


Wote pamoja watashambulia Wafilistini wanaokuwa upande wa magaribi, pamoja watawanyanganya watu wanaokaa upande wa mashariki. Watawashinda Waedomu na Wamoabu, nao Waamoni watawatii.


Mutoto muchanga atacheza kwenye shimo la nyoka, mutoto ataweza kutia mukono kwenye shimo la nyoka wa sumu.


Ulie ewe mulango; ulalamike ewe muji; tetemeka kwa hofu, ewe inchi yote ya Filistia. Maana moshi wa waaskari unakuja kutoka kaskazini, wala hakuna atakayechelewa katika makundi yake.


Sasa, ee Mungu, umewatupa watu wako, wazao wa Yakobo. Maana kweli wachawi kutoka mashariki wamejaa kati yao; kuna waaguzi kama vile kwa Wafilistini. Wanashirikiana na watu wageni.


Ujumbe wa Mungu juu ya nyama wa pande za jangwa ya kusini: Wajumbe wanapita katika inchi ya taabu na shida, yenye simba, nyoka wa sumu na nyoka wakubwa wanaoruka. Wamewabebesha punda na ngamia wao mali zao, kuwapelekea watu wasioweza kuwafalia kitu.


Hili ni neno Yawe alilomwambia nabii Yeremia juu ya Wafilistini, mbele mufalme wa Misri hajaushambulia muji wa Gaza:


Yawe amefanya yale aliyokusudia, ametimiza yale aliyoagiza. Kama alivyopanga tangu kale, ameangamiza bila huruma yoyote. Amewafanya waadui wafurahie azabu yako, amewatukuza mashujaa wa waadui zako.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa sababu Wafilistini walifanya kisasi, wakawalipiza kisasi waadui zao kwa ubaya sana na kuendelea kuwa waadui zao siku zote,


Wewe mwanadamu! Watu wa muji wa Tiro wameuchekelea Yerusalema na kusema: Aha! Yerusalema muji ambao watu wote walipitia, umeangamizwa! Sasa umetuachia nafasi; utajiri wake umeharibika!


kama wewe ulivyofanya wakati inchi ya Waisraeli ilipoharibiwa. Utakuwa jangwa, ewe mulima Seiri, pamoja na inchi yote ya Edomu. Halafu watu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Musifurahi enyi Waisraeli! Musishangilie kama watu wa mataifa mengine; maana, mumekuwa wazinzi kwa kumwacha Mungu wenu. Mumefurahia malipo ya uzinzi, kwa kila nafasi ya kupepetea ngano.


Jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa kama damu, mbele ya kutimia kwa siku ya Yawe, siku inayokuwa kubwa na ya kutisha.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Gaza, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekamata watu wengi na kuwapeleka kwa Waedomu.


Nitaondoa wakaaji wa muji wa Asidodi, pamoja na mutawala wa Asikeloni. Nitanyoosha mukono wangu kwa kuazibu muji wa Ekuroni, na Wafilistini wote waliobaki wataangamia. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Hamukupaswa kuangalia tu siku hiyo wandugu zenu walipopatwa na taabu, hamukupaswa kufurahi juu ya Wayuda siku hiyo walipoangamizwa, hamukupaswa kujivuna siku ile wenzenu walipokuwa wanateseka,


Usifurahie hali yangu ewe adui yangu! Nikianguka, nitasimama tena; nikiwa katika giza, Yawe ni mwangaza wangu.


Muji wa Gaza utahamwa, muji wa Askeloni utakuwa tupu. Wakaaji wa Asidodi watafukuzwa muchana, na wale wa Ekroni wataongolewa.


Ole wenu wakaaji wa inchi za pembeni ya bahari, watu wanaoishi kule Krete! Yawe amesema juu yenu, enyi wakaaji wa Kanana, inchi ya Wafilistini: Mimi nitawaangamiza wala hakutabaki hata mukaaji mumoja!


Siku hiyo, hautapata haya kutokana na matendo yako ya kuniasi, maana nitawaondoa kati yako wale wanaojivuna na kujitukuza, nawe hautakuwa na kiburi tena kwenye mulima wangu mutakatifu.


Muji wa Askeloni utaona hayo na kuogopa, nao muji wa Gaza utagaagaa kwa uchungu; hata Ekroni, maana tumaini lake litatoweka. Gaza utapoteza mufalme wake, nao Askeloni hautakaliwa na watu.


Halafu Yawe akamwambia Musa: Tengeneza nyoka wa shaba, umutundike juu ya muti. Mutu yeyote atakayeumwa na nyoka, akiangalia kwenye nyoka huyo wa shaba, atapona.


ni kusema eneo linalojulikana kama la Wakanana, kuanzia kwenye kijito cha Sihori kwa mupaka wa Misri mpaka kwenye eneo la Ekuroni kule kaskazini. Maeneo yote ya watawala watano wa Wafilistini: Gaza, Asidodi, Asikeloni, Gati na Ekuroni pamoja na eneo la Awini,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ