Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 14:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Kama Yawe wa majeshi ameamua, nani atakayeweza kuvunja uamuzi wake? Kama anaunyoosha mukono wake kutoa azabu, ni nani atakayemupinga?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 14:27
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

akaomba kwa sauti akisema: “Ee Yawe, Mungu wa babu zetu, wewe ndiwe Mungu unayekuwa mbinguni! Wewe unatawala falme zote katika dunia, una uwezo na nguvu, wala hakuna anayeweza kukupinga.


Kama Mungu akipita, akimufunga mutu na kumuhukumu, nani anayeweza kumuzuia?


Lakini yeye habadiliki, nani anayeweza kumugeuza? Kitu anachotaka, ndicho anachofanya!


Unataka kweli kugeuza hukumu yangu, kuniona nina kosa kusudi wewe usikuwe na kosa?


Ninajua kwamba unaweza kila kitu, lolote unalokusudia haliwezi kuzuiliwa.


Yeye akitwaa kitu kwa rafla, nani anayeweza kumuzuia? Nani anayeweza kumwuliza: “Unafanya nini?”


Mipango ya Yawe inadumu milele; kusudi lake linadumu kwa vizazi vyote.


Katika moyo wa mutu muna mipango mingi, lakini anachokusudia Yawe ndicho kitakachokamilika.


Hakuna hekima, ufahamu, wala shauri yoyote ya mutu, itakayoweza kupingana na Yawe.


Ni Yawe wa majeshi! Yeye ndiye aliyeyapanga haya yote. Alifanya hivyo akiharibu kiburi chao na kuwapatisha haya waheshimiwa wake.


Mimi ni Mungu na nitakuwa Mungu siku zote. Hakuna anayeweza kuepuka nguvu yangu; hakuna anayeweza kupinga ninayofanya.


Ninamwita tai wangu kutoka mashariki, ambaye atatimiza kusudi langu toka inchi ya mbali. Mimi nimesema na nitafanya; mimi nimepanga nami nitatimiza.


Mushauriane pamoja lakini itakuwa bure; mufanye mipango lakini haitawezekana, maana Mungu Yuko Pamoja Nasi.


Ingawa aliwaazibu watu, hawakumurudilia Yawe wa majeshi.


Kwa hiyo, inchi itaomboleza, na mbingu zitakuwa nyeusi. Maana nimesema nami sitabadilisha nia yangu; nimeamua, wala sitarudi nyuma.


Ni wachache tu ndio watakaoponyoka katika vita na kurudi kutoka inchi ya Misri na kwenda katika inchi ya Yuda. Halafu Wayuda wote waliobaki kati ya wale waliokwenda kukaa Misri watatambua ni neno la nani lenye nguvu: langu au lao!


Kwa hiyo, musikilize mupango ambao mimi Yawe nimepanga juu ya Edomu pamoja na mambo niliyokusudia kuwafanyia wakaaji wa Temani: Hakika, watoto wao wadogo watakokotwa na kukamatwa; kweli kutakuwa mushangao mukubwa katika makao yao!


Katika mwaka wa ine wa utawala wake, mufalme Zedekia alikwenda Babeli pamoja na mukubwa wa wasimamizi wa nyumba yake anayeitwa Seraya mwana wa Neria na mujukuu wa Maseya. Wakati huo mimi Yeremia nilimutolea Seraya ujumbe.


Nitakufanya kuwa kama jiwe; utakuwa pahali pa wavuvi pa kukaushia nyavu zao, wala hautajengwa tena. Mimi Yawe nimesema. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Tunajua kwamba katika mambo yote Mungu anatumika kwa kuwajalia wale wanaomupenda, ndio wale walioitwa naye kufuatana na kusudi lake.


Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ