Kwa hiyo hasira ya Yawe iliwawakia watu wake, akaunyoosha mukono wake juu yao, akawaazibu. Milima ikatetemeka, maiti zao zikakuwa kama takataka katika barabara za muji. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.
Yawe, Mungu wa Israeli, akaniambia hivi: Twaa toka katika mukono wangu kikombe hiki cha divai kinachojaa kasirani yangu uyakunyweshe mataifa yote ninayokutuma kwao.
Yawe atanyoosha mukono wake kwa kuazibu inchi ya upande wa kaskazini, na kuiangamiza inchi ya Asuria. Ataufanya muji wa Ninawe kuwa ukiwa, kuwa pahali penye kukauka kama jangwa.