Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 14:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Nitauvunja uwezo wa Waasuria katika inchi yangu; nitawakanyagakanyaga katika milima yangu. Nitawaondolea watu wangu nira yao ya unyanganyi, na muzigo wa mateso yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 14:25
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye Yawe akatuma malaika aliyewaua waaskari shujaa, majemadari na wakubwa katika kambi ya mufalme wa Asuria. Basi, mufalme wa Asuria akarudia katika inchi yake akijaa haya. Mara tu alipoingia ndani ya nyumba ya mungu wake, wana wake mwenyewe wakamwua palepale kwa upanga.


Wakati Yawe atakapomaliza kazi zake zote kwenye mulima Sayuni na katika Yerusalema, atamwazibu mufalme wa Asuria, kwa sababu ya majivuno na kiburi chake.


Yawe amelivunja gongo la waovu, ameivunja fimbo ya kifalme ya watawala,


Ole kwako! Unaangamiza ingawa hauangamizwi. Unadanganya ingawa haudanganywi. Utakapokwisha kuangamiza, wewe utaangamizwa! Utakapomaliza kudanganya, wewe utadanganywa.


Ujikungute mavumbi, usimame, ewe Yerusalema uliyekuwa mufungwa! Ujifungue minyororo yako katika shingo, ewe binti Sayuni uliyekamatwa mateka.


Viatu vyote vya washambulizi katika vita na nguo zote zenye kujaa damu vitateketezwa kama kuni za kuwasha moto.


Asuria iko huko. Makaburi ya waaskari wake yanaizunguka. Wote waliuawa katika vita.


Utakufa juu ya milima ya Israeli, wewe pamoja na makundi yako yote ya waaskari na mataifa yanayokuwa pamoja nawe. Nami nitaitoa miili yao ikuliwe na ndege wa kila aina na nyama wakali.


Kwa silaha zao wataitawala inchi ya Asuria, na kuirizi inchi ya Nimurodi. Watatuokoa toka katika mikono ya Waasuria, watakapoingia katika inchi yetu na kuanza kuishambulia.


Wazao wa Yakobo watakaobaki wazima wataenea kati ya mataifa mengi, watakuwa kama umande unaotoka kwa Yawe, kama manyunyu yanayoanguka kwenye majani ambayo hayasababishwi na mutu wala kumutegemea mwanadamu.


Sasa nitaivunja nira ya Asuria katika shingo lenu, na minyororo waliyowafungia nitaikatakata.


Watapitia katika bahari ya mateso, nami nitayapiga mawimbi yake, na vilindi vya maji ya muto Nili vitakauka. Kiburi cha Asuria kitavunjwa na nguvu za Misri zitatoweka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ