Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 14:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Yawe wa majeshi ameapa: Kama nilivyopanga, ndivyo itakavyokuwa; kama nilivyokusudia, ndivyo itakavyokamilika.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 14:24
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ndoto yako ilirudiliwa mara mbili kwa mifano inayofanana kwa kukuonyesha kwamba Mungu ameamua, naye atatimiza jambo hili sasa hivi.


Lakini yeye habadiliki, nani anayeweza kumugeuza? Kitu anachotaka, ndicho anachofanya!


Yawe amekuapia hivi wala hatabadilisha nia yake: “Wewe ni kuhani milele kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.”


Yawe anavunja mipango ya mataifa, na anabadilisha mawazo yao.


Ee Yawe, matendo yako makubwa yananifurahisha; nitashangilia kwa sababu ya mambo yote uliyotenda.


akisema: “Muinue juu bendera ya Yawe! Yawe atapigana na Waamaleki kizazi kwa kizazi!”


Katika moyo wa mutu muna mipango mingi, lakini anachokusudia Yawe ndicho kitakachokamilika.


Hakuna hekima, ufahamu, wala shauri yoyote ya mutu, itakayoweza kupingana na Yawe.


Ole kwake Asuria, yeye ni kama fimbo ya hasira yangu, yeye anayeshika kiboko cha hasira yangu!


Wako wapi, ewe Mufalme wa Misri, wenye hekima wako? Uwaache basi wakwambie na kukujulisha mambo Yawe wa majeshi aliyopanga juu ya Misri!


Yuda atakuwa kitisho kikubwa kwa Wamisri. Wote watakaoambiwa habari za Yuda wataingiwa na woga kwa sababu ya jambo Yawe wa majeshi aliloamua kuwatendea.


Maana mawazo yangu si kama mawazo yenu, wala njia zangu si kama njia zenu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Kama vile mbingu zinavyokuwa mbali na dunia, ndivyo njia zangu zinavyokuwa mbali na zenu, na mawazo yangu mbali na mawazo yenu.


Hasira ya Yawe haitatulia, mpaka atakapotimiza na kukamilisha mapenzi ya moyo wake. Kutakuja siku ambapo mutaelewa vema mambo hayo.


Maana, mimi ninajua mupango ninaokuwa nao juu yenu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nayo mipango yangu ni ya kuwatendea mema wala si mabaya, kusudi mupate kuwa na tumaini katika siku zinazokuja.


Lakini musikilize neno la Yawe, enyi watu wote wa Yuda munaokaa katika inchi ya Misri. Yawe anasema hivi: Ninaapa kwa jina langu kubwa kwamba hakuna mutu yeyote wa Yuda katika inchi yote ya Misri atakayelitumia jina langu kwa kuapa nalo akisema: Kama vile Bwana wangu Yawe anavyoishi.


Kwa hiyo, musikilize mupango ambao mimi Yawe nimepanga juu ya Edomu pamoja na mambo niliyokusudia kuwafanyia wakaaji wa Temani: Hakika, watoto wao wadogo watakokotwa na kukamatwa; kweli kutakuwa mushangao mukubwa katika makao yao!


Kwa hiyo, musikilize mupango ambao Yawe amepanga juu ya Babeli pamoja na mambo aliyokusudia kuifanyia inchi ya Wakaldea: Hakika, watoto wao wadogo watakokotwa na kukamatwa; kweli kutakuwa mushangao mukubwa katika makao yao!


Nani anayeweza kusema kusudi kitu kifanyike ikiwa Yawe asipoamuru ikuwe hivyo?


Mimi Yawe mwenyewe nitatangaza yatakayotukia. Nayo yatatukia bila kukawia. Wakati ninyi mungali munaishi, enyi watu waasi, neno nitakalosema nitalitimiza. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Utakufa juu ya milima ya Israeli, wewe pamoja na makundi yako yote ya waaskari na mataifa yanayokuwa pamoja nawe. Nami nitaitoa miili yao ikuliwe na ndege wa kila aina na nyama wakali.


Baragumu ya vita inalia katika muji bila kutia watu hofu? Muji unaweza kupatwa na hasara ambayo haikuletwa na Mungu?


Yawe, utukufu wa Yakobo, ameapa: Hakika, sitayasahau matendo yao maovu.


Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.


Hivi walitimiza mambo uliyokuwa umekusudia tangu zamani kwa uwezo wako na kwa mapenzi yako.


Ametujulisha mipango yake iliyokuwa imefichwa; ndiyo ile aliyokusudia kwa mapenzi yake tangu mbele kwamba ataitimiza kwa njia ya Kristo.


Lakini sasa sisi tulioamini, tutaingia kwenye mapumziko ambayo Mungu alitaja aliposema: “Halafu nikaapa kwa kasirani kwamba hawataingia hata kidogo kwenye mapumziko niliyowatayarishia!” Mungu alisema vile ingawa alikuwa amemaliza kazi zake tangu pale alipoumba dunia.


Ilikuwa ni mapenzi ya Yawe mwenyewe kuifanya mioyo ya watu wa mataifa hayo kuwa migumu kusudi wapigane. Alikusudia wasihurumiwe lakini wateketezwe. Ndivyo Yawe alivyomwamuru Musa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ