Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 14:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Lakini wewe umetupwa inje ya kaburi lako, kama mutoto wa kuchukiza aliyezaliwa mufu, kama maiti ambayo imekanyagwakanyagwa. Umelundikiwa maiti za waliouawa kwa upanga, waliotupwa ndani ya mashimo penye mawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 14:19
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Umwambie, Yawe anasema hivi: ‘Umeua na kutwaa mali yake vilevile?’ Umwambie Yawe anasema hivi: ‘Pahali pale imbwa walipoilambulia damu ya Naboti, ndipo watakapoilambulia damu yako.’ ”


Hakika, mutu yeyote wa jamaa yake atakayekufia ndani ya muji, imbwa watamukula; na mutu yeyote atakayekufia katika shamba, ndege watamukula.’ ”


Yehu akamwambia musaidizi wake Bidikari: “Kamata hiyo maiti yake uitupe katika shamba hilo la Naboti wa Yezereheli. Kwa maana, kumbuka wewe na mimi tulipokuwa tumepanda juu ya farasi wetu nyuma ya baba ya Ahabu, jinsi Yawe alivyosema maneno haya juu yake.


Yeyote atakayeonekana atapigwa mukuki, atakayekamatwa atauawa kwa upanga.


Wafalme wote wa mataifa wamezikwa kwa heshima kila mumoja ndani ya kaburi lake.


Maiti zao zitatupwa inje; harufu ya maiti zao itasambaa; damu yao itatiririka juu ya milima.


Kwa hiyo hasira ya Yawe iliwawakia watu wake, akaunyoosha mukono wake juu yao, akawaazibu. Milima ikatetemeka, maiti zao zikakuwa kama takataka katika barabara za muji. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Wote, wakubwa kama vile wadogo, watakufa katika inchi hii; nao hawatazikwa, wala hakuna atakayeomboleza juu yao. Hakuna atakayejikatakata wala kunyolewa upaa kwa ajili ya kifo chao.


Yeye atazikwa sawa nyama: atakokotwa na kutupiliwa mbali, inje ya milango ya Yerusalema.


Walipoingia katika muji, Isimaeli mwana wa Netania, pamoja na wale watu kumi waliokuwa pamoja naye, waliwaua watu hao na kuzitupa maiti zao ndani ya kisima.


Kisima ambamo Isimaeli alitupa maiti za wale watu aliowaua ni kile kikubwa ambacho mufalme Asa alikuwa amekichimba kwa kujikinga na Basha, mufalme wa Waisraeli. Isimaeli mwana wa Netania alikijaza kisima hicho maiti za wale watu aliowaua.


Wataanguka na kuuawa katika inchi ya Wakaldea, wataumizwa katika barabara zake.


Makaburi yao yako sehemu za chini kabisa katika shimo kwa wafu. Waaskari wao wanaizunguka. Wote waliuawa katika vita. Walipokuwa wangali wanaishi, walieneza vitisho vyao katika inchi ya wanaokuwa wazima.


Hawakuzikwa pamoja na mashujaa wa zamani, ambao walikwenda katika kuzimu kwa wafu wakiwa na silaha zao, mapanga yao chini ya vichwa vyao na ngao zao juu ya miili yao. Mashujaa hao walipokuwa wangali wanaishi walijaza vitisho vyao katika inchi ya wanaokuwa wazima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ