Wakamuzika katika muji wa Daudi, kwenye makaburi ya wafalme kwa kuonyesha heshima yao kwake kwa sababu alifanya mema katika Israeli na mbele ya Mungu na nyumba yake.
Waadui walipoondoka, wakamwacha akiwa ameumizwa vibaya sana, wakubwa wake wakamufanyia shauri baya, wakamwua juu ya kitanda chake, kwa kulipiza kisasi cha mauaji ya mwana wa kuhani Yoyada. Alizikwa katika muji wa Daudi, lakini si kwenye makaburi ya wafalme.
watu wanaogopa mupando na kutishwa katika njia, muti wa lozi unachanua maua yake meupe, mapanzi hayawezi kuruka, hakuna hamu tena, mwanadamu anaelekea kwenye makao yake ya milele, waombolezaji wanasambaa katika njia,
Mutu akiweza kuzaa watoto mia moja, na akiishi maisha marefu, lakini kama mutu huyo hafurahii maisha yake, wala hafanyiwi mazishi, basi ninasema mutoto aliyezaliwa amekufa ni afazali kuliko mutu yule.
Lakini wewe umetupwa inje ya kaburi lako, kama mutoto wa kuchukiza aliyezaliwa mufu, kama maiti ambayo imekanyagwakanyagwa. Umelundikiwa maiti za waliouawa kwa upanga, waliotupwa ndani ya mashimo penye mawe.