Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 14:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Wewe ulijisemesha ndani ya moyo wako: Nitapanda mpaka mbinguni; nitaweka kiti changu juu ya nyota za Mungu, nitaikaa juu ya mulima pahali miungu wanapokutana, huko mbali pande za kaskazini.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 14:13
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mwovu akiweza kupanda hata kufikia mbingu, na kichwa chake kufika kwenye mawingu,


Yawe, ni mukubwa; anastahili kusifiwa sana katika muji wake, ndio mulima wake mutakatifu.


Katika siku zinazokuja, itatukia kwamba mulima wa nyumba ya Yawe utaimarishwa kupita milima yote, utainuliwa juu ya vilima vyote. Mataifa yote yatajaa kule,


Vitisho unavyotoa na kiburi chako vimekudanganya, ewe unayekaa katika mapango ya mawe, unayeishi juu ya kilele cha mulima! Ingawa unaweka makao yako juu kama ya tai, mimi nitakuporomosha kutoka huko unakokuwa. –Ni ujumbe wa Yawe.


Muji wenye kuwa karibu ya bahari, unaofanya biashara na mataifa ya visanga vingi. Umwambie: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ewe Tiro, wewe umejivuna kuwa muzuri kwelikweli!


Wewe mwanadamu! Umwambie mufalme wa Tiro kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Wewe una kiburi cha moyo, na umesema kwamba wewe ni mungu, kwamba umeikalia kiti cha kifalme cha miungu, umekaa mbali huko katika bahari. Lakini, wewe ni mutu tu wala si mungu, ingawa unajiona kuwa na hekima kama mungu.


Utaendelea kujiona kuwa mungu mbele ya hao watakaokuua? Katika mikono ya hao watakaokuangamiza, utatambua kwamba wewe ni mutu tu, wala si mungu!


Umwambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana na wewe mufalme wa Misri, wewe mamba unayelala ndani ya muto Nili! Wewe unafikiri kwamba muto Nili ni wako, kwamba wewe ndiwe uliyeufanya!


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa sababu ulirefusha kimo chake na kufikisha kilele chake katika mawingu makubwa, ukajivunia urefu wake,


Basi, nikiwa katika maono Yawe akanipeleka mpaka katika inchi ya Israeli, akaniweka juu ya mulima murefu sana, na upande wa kusini kulikuwa majengo yaliyoonekana kama muji.


Mufalme atafanya kama anavyopenda. Atajitukuza na kujivuna kwamba yeye ni mukubwa kuliko miungu yote, na kumutukana Mungu wa miungu. Ataendelea kufanikiwa mpaka kasirani ifikie ukomo wake, maana yaliyopangwa sherti yatimie.


Lakini alipoanza kuwa na kiburi, akakuwa na roho ngumu na mwenye majivuno, aliondolewa katika kiti chake cha kifalme, akanyanganywa utukufu wake.


Kiburi chako kimekudanganya: wewe unayekaa ndani ya mashimo chini ya mawe makubwa na makao yako yapo juu kwenye milima, hivyo unajisemesha: Nani anayeweza kunishusha chini?


Basi huu ndio muji uliojivuna na kuishi kwa usalama, muji uliojisemesha: Ni mimi tu, hakuna mwingine! Jinsi gani umekuwa mutupu na makao ya nyama wa pori! Kila mutu anayepita karibu atauzomea na kuuzarau.


Nawe, muji Kapernaumu, unafikiri kwamba utapandishwa mpaka juu mbinguni? Utashushwa mpaka chini katika kuzimu. Kwa maana miujiza iliyofanyika ndani yako ingalifanyika katika Sodoma, muji ule ungekuwa ungali hata leo.


Nawe muji Kapernaumu, unafikiri kwamba utapandishwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka chini katika kuzimu.”


Yeye atapinga kitu chochote watu wanachohesabu kuwa cha kimungu au wanachoabudu na kujiweka kuwa juu ya vyote. Yeye ataenda hata kuingia katika hekalu la Mungu na kukaa mule na kujiita mwenyewe kuwa Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ