Maana hakuna anayemukumbuka mwenye hekima, wala anayemukumbuka mupumbafu, maana katika siku zinazokuja wote watasahaulika. Maana mwenye hekima anakufa sawasawa na mupumbafu!
Nitakuteremusha ndani ya shimo kusudi ujiunge na wale wanaokuwa huko, walioishi zamani katika dunia; utakaa kule katika matongo kwa milele. Hautakaliwa na watu milele na hautakuwa na nafasi katika inchi za wanaokuwa wazima.
Wakubwa wenye nguvu pamoja na wasaidizi wao wakiwa huko katika shimo kwa wafu watasema hivi: Wamisri wameshuka chini kwa wafu, wanalala pamoja na watu wasiomujua Mungu, waliouawa katika vita.