Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 13:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Siku ya Yawe inakuja, siku kali, ya kasirani na hasira kali. Itaifanya inchi kuwa uharibifu, itawaangamiza wenye zambi ndani yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 13:9
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wenye zambi wote waondolewe katika dunia, waovu wote wasikuwe tena! Umusifu Yawe, ee nafsi yangu! Haleluia!


Lakini waovu wataondolewa katika inchi, na watu wabaya watangolewa toka ndani yake.


Mulie, maana siku ya Yawe imekaribia; inakuja kama uharibifu kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu.


Kweli, siku ya Yawe wa majeshi inakuja juu ya wote wenye kiburi na majivuno, juu ya wote wanaojitukuza,


Maana Yawe yuko na siku ya kulipiza kisasi; mwaka wa kulipiza waadui za Sayuni.


Niliamua kwamba siku ya kulipiza kisasi imefika; wakati wa kuwakomboa watu wangu umefika.


Kuna watu wanaojitakasa na kujisafisha wapate kuingia kwenye bustani za ibada za sanamu; wanafanya maandamano na kuhani akiwa kati yao. Watu wale wanakula nguruwe, panya na vyakula vingine vyenye kuwa machukizo. Watu wale hakika watakufa wote pamoja. –Ni ujumbe wa Yawe.–


wananyanganya upande mumoja na hawatosheki; wanakula upande mwingine lakini hawashibi. Kila mumoja anamushambulia mwenzake.


Hawakwenda kulinda sehemu zile za kuta zilizobomoka wala hawajengi kuta mupya kusudi Waisraeli waweze kujilinda wakati wa vita siku ile ambayo mimi Yawe nimeiweka.


Kwa maana, siku hiyo imekaribia; siku ile ya Yawe iko karibu. Hiyo itakuwa siku ya mawingu ya kutisha, siku ya maangamizi kwa mataifa.


Ole kwetu kwa ile siku ya Yawe, siku hiyo ya Yawe inakaribia; inakuja pamoja na maangamizi, kutoka kwa Mungu Mukubwa.


Mupige baragumu kule Sayuni; mupige kelele la kujulisha hatari kule juu ya mulima mutakatifu! Mutetemeke enyi wakaaji wa Yuda, maana siku ya Yawe inakuja, siku hiyo iko karibu!


Yawe ni Mungu mwenye wivu, anayelipiza kisasi; Yawe analipiza kisasi na ni mwenye kasirani; Yawe analipiza kisasi kwa wapinzani wake, kasirani yake inawaka juu ya waadui zake.


Nani anayeweza kusimama mbele ya kasirani ya Yawe? Nani anayeweza kuvumilia ukali wa hasira yake? Yeye anaimwanga hasira yake inayowaka kama moto, hata mawe makubwa anayapasua vipandevipande.


Waadui wakishambulia inchi kama mafuriko, yeye anawaangamiza; anawafuatilia na kuwafukuza mpaka katika giza.


Siku hiyo itakuwa siku ya kasirani, ni siku ya taabu na uchungu, siku ya giza na huzuni; siku ya uharibifu na maangamizi, siku ya mawingu na giza kubwa.


Angalia, siku ya kasirani ya Yawe inakuja. Siku hiyo, enyi watu wa Yerusalema, mali yenu itagawanywa mbele ya macho yenu.


Kwa sababu hiyo, kwa muda wa siku moja tu utapatwa na mapigo ya mauti, huzuni na njaa. Na zaidi ya hiyo utateketezwa kwa moto, kwa maana Bwana wetu, Mungu anayeuhukumu, ni mwenye uwezo.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ