Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 13:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Watu watafazaika, watashikwa na hofu na maumivu, watakuwa na uchungu kama mama anapozaa. Wataangalia kwa mashaka, nyuso zao zitaungua kwa haya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 13:8
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakaaji wake wakiwa wameishiwa nguvu, wametishika na kufazaika, wamekuwa kama mimea ya shamba, kama majani changa, kama majani yanayoota juu ya paa, yanayokauka mbele ya kukomaa.


Hofu kubwa iliwashika, wakasikia uchungu kama mama anayezaa,


Kama vile mama mwenye mimba anayezaa analia na kugaagaa kwa uchungu, ndivyo tulivyokuwa kwa sababu yako, ee Yawe.


Utasema nini juu ya wale uliowazoeza kuwa warafiki zako, wale ambao wewe mwenyewe uliwafundisha, watakapokushinda na kukutawala? Si utashikwa na uchungu sawa vile mwanamuke anayezaa?


Mujiulize sasa na kufahamu: Mwanaume anaweza kuzaa mutoto? Mbona basi, ninamwona kila mwanaume anajikamata kwenye kiuno kama mwanamuke anayesikia maumivu ya kuzaa na nyuso zimebadilika?


Nilisikia sauti kama ya mwanamuke anayezaa, malalamiko kama ya mwenye kuzaa mutoto wa kwanza. Ilikuwa sauti ya Yerusalema akipumuapumua kwa uchungu, na kuinyooshanyoosha mikono yake, akisema: Ole wangu! Wanakuja kuniua!


Lakini mbona ninawaona wametishwa? Wamerudi nyuma. Mashujaa wao wamepigwa, wamekimbia mbio, bila hata kuangalia nyuma. Kuna kitisho kila upande. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Miji yake itatekwa, kuta zake vilevile. Siku hiyo mioyo ya waaskari wa Moabu itakuwa kama vile moyo wa mwanamuke anayezaa.


Adui atapanda juu na kuruka kama tai na kutandaza mabawa yake juu ya Bosira. Siku hiyo moyo wa mashujaa wa Edomu utakuwa kama vile moyo wa mwanamuke anayezaa.


Watu wa Damasiki wamevunjika moyo; wamegeuka kusudi wapate kukimbia; hofu kubwa imewashika, uchungu na huzuni vimewapata, kama mwanamuke anayezaa.


Mufalme wa Babeli amesikia habari zao. Kwa hiyo, mikono yake ikaregea. Ameshikwa na huzuni na uchungu, kama mama anayezaa.


Waaskari wa Babeli wameshindwa kupigana, wamebaki katika makimbilio yao; nguvu zao zimewaishia, wamekuwa kama wanawake. Nyumba za Babeli zimechomwa kwa moto, milango yake ya chuma imevunjwa.


Maumivu kama ya kuzaa mutoto yanamufikia. Lakini yeye ni mutoto mupumbafu; wakati wa kuzaliwa unapofika yeye anakataa kutoka ndani ya tumbo la mama!


Wanapokaribia, watu wanajaa hofu, nyuso zao zinawaivya.


Munyanganye feza, munyanganye zahabu! Mali yake haina mwisho! Kuna wingi wa kila kitu cha bei kali!


Wakati mwanamuke anapozaa, anasikia uchungu kwa sababu wakati wake wa kuzaa umetimia. Lakini anapokwisha kuzaa, hakumbuki tena maumivu, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa kwa mutoto.


Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ