Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 13:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Hautakaliwa tena na watu hata kidogo, watu hawataishi humo katika vizazi vyote. Hakuna Mwarabu atakayesimamisha hema yake humo, wala muchungaji atakayechunga nyama wake humo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 13:20
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Vilevile Wafilistini wamoja wakamuletea Yosafati zawadi pamoja na feza nyingi na Waarabu wengine nao wakamuletea kondoo dume elfu saba na mia saba, na mbuzi dume elfu saba na mia saba.


Usiku ule ukuwe tasa, sauti ya furaha isiingie ndani yake.


Basi uniambie ee wangu wa moyo, utawakulishia kondoo wako wapi? Ni wapi watakapopumzikia pa saa sita? Kwa nini mimi nikutafute kati ya makundi ya wenzako?


Nitaufanya kuwa makao ya nungunungu, na utakuwa tingitingi ya maji. Nami nitaufagilia mbali kwa ufagio wa maangamizi. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.


Ujumbe wa Mungu juu ya jangwa kando ya bahari. Kama upepo mukali unaovuma kutoka kusini, washambulizi wanakuja kutokea katika jangwa, kutoka katika inchi ya kutisha.


Umeufanya muji kuwa lundo la mawe, muji wenye pango kuwa uharibifu. Nyumba za watu wageni zimetoweka, wala hazitajengwa tena upya.


Yawe amepanga sehemu ya kila mumoja wao, ametumia kamba kuwapimia inchi hiyo; watairizi milele na milele, wataishi mule kizazi hata kizazi.


Muji wa Hazori utakuwa makao ya mbweha, utakuwa jangwa siku zote; hakuna mutu atakayekaa humo, wala atakayeishi humo.


Kwa sababu ya kasirani yangu Yawe, Babeli haitakaliwa kabisa na watu, lakini itakuwa jangwa kabisa; kila mutu atakayepita karibu nayo atashangaa, ataizomea kwa sababu ya mapigo yake.


Mupande, muiendee inchi ya Merataimu, muende kuishambulia; muwashambulie wakaaji wa Pekodi na kuwaangamiza kabisa watu wake. –Ni ujumbe wa Yawe.– Mufanye kila kitu nilichowaamuru.


Kwa maana, taifa kutoka kaskazini limefika kuushambulia; litaifanya inchi yake kuwa uharibifu. Hakuna atakeyeishi humo; watu na nyama watakimbia mbali.


Kwa hiyo nyama wa pori, imbwa wa pori pamoja na mbuni, watakaa Babeli. Hakutakaliwa hata kidogo na watu wa vizazi vyote vinavyokuja.


Kwa hiyo, musikilize mupango ambao Yawe amepanga juu ya Babeli pamoja na mambo aliyokusudia kuifanyia inchi ya Wakaldea: Hakika, watoto wao wadogo watakokotwa na kukamatwa; kweli kutakuwa mushangao mukubwa katika makao yao!


Mimi ninapingana nawe, ewe mulima muharibifu, mulima unaoharibu dunia nzima! –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitanyoosha mukono wangu juu yako kwa kukuazibu, nitakuangusha kutoka juu kwenye mawe makubwa na kukufanya kuwa mulima uliochomwa kwa moto.


Inchi inatetemeka na kugaagaa kwa maumivu, maana nia ya Yawe juu ya Babeli ni imara: ataifanya inchi ya Babeli kuwa jangwa, ataifanya ikuwe bila watu.


Babeli itakuwa lundo la mabomoko, itakuwa makao ya mbweha, itakuwa machukizo na kitu cha kuzomewa; hakuna mutu atakayekaa ndani yake.


Miji yake imekuwa ukiwa, inchi yenye kukauka na jangwa, inchi isiyokaliwa na mutu yeyote, wala hakuna mwanadamu yeyote anayepita ndani yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ