Hazaeli akamwuliza: “Bwana wangu, mbona unalia?” Elisha akamujibu: “Kwa sababu ninajua maovu ambayo utawatendea watu wa Israeli. Utateketeza kuta zao kwa moto, na kuwaua vijana wao, utawapondaponda watoto wao na kupasua wanawake wenye mimba tumbo.”
Kwa hiyo, Yawe alimuleta mufalme wa Wakaldea ambaye aliwaangamiza vijana wao kwa upanga hata ndani ya Pahali Patakatifu; wala hakumuhurumia mutu yeyote akuwe kijana au binti, muzee au muzaifu. Wote Yawe aliwatia katika mikono yake.
Haya yote mawili yatakupata kwa rafla katika siku moja: kupoteza watoto wako na kuwa mujane, ijapokuwa una wingi wa uchawi wako, na nguvu nyingi za uganga wako.
Mishale yao ni mikali sana, pinde zao zimevutwa tayari. Kwato za farasi wao ni ngumu kama mawe; mwendo wa magurudumu ya magari ni kama wa upepo mukali.
Kwa hiyo uwaache watoto wao wakufe kwa njaa, uwaache wakufe kwa vita. Wake zao wakuwe tasa na wajane. Waume zao wakufe kwa magonjwa makali na vijana wao wachinjwe kwa upanga katika vita.
Wameshika pinde zao na mikuki; ni watu wakali wasiokuwa na huruma. Vishindo vyao ni kama uvumi wa bahari, wamepanda juu ya farasi. Wamejipanga tayari kwa vita na wewe Babeli!
Wameshika pinde zao na mikuki; ni watu wakali wasiokuwa na huruma. Vishindo vyao ni kama uvumi wa bahari. Wamepanda juu ya farasi, wamejipanga tayari kwa vita na wewe Sayuni!
Nyama wa pili alikuwa kama dubu ambaye upande wake mumoja ulikuwa umeinuka. Na katika kinywa chake alikuwa na mifupa mitatu ya mbavu aliyoishika kwa meno yake. Sauti ikamwambia: Simama, ukule nyama nyingi kadiri unavyoweza.
Enyi watu wa Yuda muangalie: Mutu anakuja kutoka milima anayeleta habari njema, anayetangaza amani. Mufanye sikukuu zenu, mutimize viapo vyenu, maana waovu hawatawashambulia, kwa sababu wameangamizwa kabisa.
Hata hivyo, ulikamatwa mateka, watu wake wakapelekwa katika uhamisho. Hata watoto wake walipondwapondwa katika maingilio ya kila barabara; watu wake wenye heshima waligawanywa kwa kuwapigia kura, wakubwa wake wote walifungwa minyororo.