Katika taabu yangu, nilimwita Yawe; nilimulilia Mungu wangu anisaidie. Toka katika hekalu lake, alisikia sauti yangu; kilio changu kilimufikia katika masikio yake.
Muingie katika mapango chini ya mawe, katika mashimo ndani ya udongo, kwa kuepuka kitisho cha Yawe, mbali na mwangaza wa utukufu wake, atakapokuja kuogopesha dunia.
Ujumbe wa Mungu juu ya jangwa kando ya bahari. Kama upepo mukali unaovuma kutoka kusini, washambulizi wanakuja kutokea katika jangwa, kutoka katika inchi ya kutisha.
Mutu atakayekimbia sauti ya woga atatumbukia ndani ya shimo; na mutu atakayetoka ndani ya shimo atanaswa katika mutego. Madirisha ya mbinguni yamefunguliwa, misingi ya dunia inatikisika.
Shuka, uikae katika mavumbi, ewe bikira, binti wa Babeli! Ikaa chini pasipo kiti cha kifalme, ewe binti wa Wakaldea! Tokea sasa hautaitwa tena murembo wala mwenye kupendeza.
Muinue macho, muangalie mbingu, kisha muangalie dunia kule chini. Mbingu zitatoweka kama moshi, dunia itachakaa kama nguo, na wakaaji wake watakufa kama vidudu. Lakini wokovu ninaouleta unadumu milele; ukombozi wangu hautakoma hata kidogo.
Enyi wapita njia wote, hivi hamujali kitu? Muangalie, muone kama kuna aliyepatwa na uchungu kama mimi, uchungu Yawe alioniletea siku ya hasira yake kali.
“Mara moja kisha mateso ya siku zile, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka toka mbinguni na vyote vyenye nguvu katika mbingu vitatikiswa.
Siku Bwana atakaporudi, itatimia kama vile mwizi anavyokuja. Siku ile mbingu zitatoweka kwa shindo kubwa, na viumbe vyote vinavyoangaza katika mbingu vitayeyuka. Dunia na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake vitateketezwa.