Kwa sababu hiyo laana inaiteketeza dunia, wakaaji wake wanateseka kwa ajili ya makosa yao. Wakaaji wa dunia wamepunguka, ni watu wachache tu waliobaki.
Wakati huo wanawake saba watashikamana na mwanaume mumoja na kumwambia: Chakula na mavazi tutajitafutia wenyewe, lakini wewe utuondolee haya yetu, uturuhusu tuitwe kwa jina lako.
Mimi nikauliza: Bwana, mpaka wakati gani? Naye akanijibu: Mpaka wakati miji itakapobaki tupu bila wakaaji, nyumba bila watu, na inchi itakapoharibiwa kabisa.