Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 13:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Nyota na vikundi vyake katika anga hazitaangaza; jua linapochomoza litakuwa giza, na mwezi hautatoa mwangaza wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 13:10
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Anaamuru jua lisipande, anafunika nyota zisiangaze.


Kwa wakati huu wa nyuma, jua, mwangaza, mwezi na nyota hazionekani tena, mawingu yanarudia nyuma ya mvua,


Siku ile Yawe ataliazibu jeshi la anga vilevile na wafalme wa dunia.


Kisha mwezi utafezeheka, nalo jua litapata haya ya kuangaza, maana Yawe wa majeshi atatawala kule Yerusalema katika mulima Sayuni; ataonyesha wazee wa watu wake utukufu wake.


Ikaa kimya, ingia katika giza, ewe taifa la Wakaldea. Maana umepoteza cheo yako ya kuwa malkia wa falme.


Siku hiyo, watanguruma juu ya Israeli kama uvumi wa bahari iliyochafuka. Atakayeiangalia inchi kavu ataona giza tupu na taabu, mwangaza utafunikwa na mawingu.


Mimi ninafunika anga kwa giza, na kulivalisha nguo ya kilio.


Inchi inatetemeka mbele yao, mbingu zinatikisika. Jua na mwezi vinatiwa giza, nazo nyota zinaacha kuangaza.


Siku ya Yawe itakuwa giza, na si mwangaza; itakuwa giza kubwa bila mwangaza wowote.


Waadui wakishambulia inchi kama mafuriko, yeye anawaangamiza; anawafuatilia na kuwafukuza mpaka katika giza.


Wakati ule hakutakuwa baridi wala baridi kali.


“Mara moja kisha mateso ya siku zile, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka toka mbinguni na vyote vyenye nguvu katika mbingu vitatikiswa.


“Lakini katika siku zile kisha mateso yale, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza,


“Vitambulisho vitaonekana katika jua, mwezi na nyota. Na hapa katika dunia mataifa yatakuwa na uchungu, na kushikwa na wasiwasi kwa ajili ya mungurumo na musukosuko wa bahari.


Jua litatiwa giza, mwezi utakuwa kama damu, mbele ya kutimia kwa siku ya Bwana, ile siku kubwa na ya utukufu.


Kisha malaika wa ine akapiga baragumu. Sehemu moja ya tatu ya jua ikaharibishwa pamoja na sehemu moja ya tatu ya mwezi na ya nyota. Sehemu zile tatu zikaingiwa na giza. Hivi hakukuwa mwangaza kwa muda wa sehemu moja ya tatu ya saa za muchana na sehemu moja ya tatu ya saa za usiku vilevile.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ