Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 13:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Haya ni maono, ambayo nabii Isaya mwana wa Amozi, aliyofunuliwa na Mungu juu ya inchi ya Babeli:

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 13:1
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yehu akamwambia musaidizi wake Bidikari: “Kamata hiyo maiti yake uitupe katika shamba hilo la Naboti wa Yezereheli. Kwa maana, kumbuka wewe na mimi tulipokuwa tumepanda juu ya farasi wetu nyuma ya baba ya Ahabu, jinsi Yawe alivyosema maneno haya juu yake.


Haya ni maono Isaya mwana wa Amozi, aliyoyaona juu ya inchi ya Yuda na Yerusalema, katika nyakati za utawala wa wafalme hawa wa Yuda: Ahazi na Hezekia.


Babeli ni utukufu wa falme zote na sifa na majivuno ya Wakaldea utakuwa kama Sodoma na Gomora, wakati Mungu alipoiangamiza.


Mwaka mufalme Ahazi alipokufa, Mungu alitoa ujumbe huu:


Ujumbe wa Mungu juu ya inchi ya Moabu. Muji wa Ari katika inchi ya Moabu umeangamizwa usiku; muji wa Kiri katika inchi ya Moabu umeangamizwa usiku.


Ujumbe wa Mungu juu ya muji wa Damasiki. Damasiki utakoma kuwa muji; utakuwa lundo la mabomoko.


Ujumbe wa Mungu juu ya inchi ya Misri. Yawe amepanda juu ya wingu linaloenda mbio na kuja mpaka katika inchi ya Misri. Sanamu za miungu ya Wamisri zitatetemeka mbele yake, mioyo ya Wamisri itayeyuka kwa woga.


Miaka mitatu mbele ya pale, Yawe alimwambia Isaya mwana wa Amozi hivi: Kwenda uvue nguo ya gunia uliyokuwa umevaa katika kiuno, na viatu vyako. Isaya akafanya kama alivyoambiwa; akakuwa anatembea uchi na bila viatu.


Ujumbe wa Mungu juu ya Arabia. Enyi makundi ya wasafiri ya Dedani, mupige kambi leo usiku katika pori za Arabia.


Ujumbe wa Mungu juu ya Bonde la Maono. Kuna nini, ee Yerusalema? Mbona watu wote mumepanda juu ya nyumba?


Lakini siku moja, –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi– ule musumari uliopigiliwa pahali pagumu utaregea kwa uzito. Utakatwa na kuanguka. Yawe amesema.


Yawe, Mukombozi wenu, Mutakatifu wa Israeli, anasema hivi: Kwa ajili yenu nitatuma waaskari kwenda Babeli. Nitavunja vifungio vya milango ya muji wake, na kelele za wale Wakaldea zitageuka maombolezo.


Ilikuwa nyuma ya Nebukadneza mufalme wa Babeli kuwahamisha Yekonia mufalme wa Yuda mwana wa Yoyakimu, pamoja na wakubwa wa inchi ya Yuda na wafundi bora na wafuaji wa vyuma kutoka Yerusalema na kuwapeleka Babeli. Yawe akanionyesha vikapu viwili vya matunda ya tini vimewekwa mbele ya hekalu la Yawe.


Manabii waliotangulia mbele yetu, mimi na wewe, zamani za kale walitabiri kwamba vita, njaa na magonjwa makali vitazipata inchi nyingi na tawala kubwa.


Yawe akatoa ujumbe huu kwa njia ya nabii Yeremia juu ya inchi ya Babeli, ile inchi ya Wakaldea:


Ninyi munasema: Tumepatishwa haya na kutukaniwa; haya imefunika nyuso zetu, kwa sababu wageni wameingia katika sehemu takatifu za nyumba ya Yawe.


Uwaambie: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Neno langu hili linaelekea mambo yatakayomupata mutawala wa Yerusalema na Waisraeli wote wanaoishi humo.


PERESI: ufalme wako umegawanywa kati ya Wamedi na Wapersi.


Basi, mufalme akabadilika rangi na kufazaika kwa ajili ya mawazo yaliyomufikia, viungo vyake vikaregea na magoti yakaanza kutetemeka.


Ujumbe wa Mungu juu ya Ninawe. Kitabu cha maono ya Nahumu wa Elkosi.


Haya ni maono ambayo nabii Habakuki aliyofunuliwa na Mungu.


Ujumbe wa Yawe unaoelekea Israeli. Yawe aliyezitandaza mbingu, aliyeiweka misingi ya dunia na kumupa mwanadamu uzima anasema hivi:


Ujumbe wa Yawe: Neno la Yawe ni juu ya azabu ya miji Hadiraki na Damasiki. Maana inchi ya Aramu ni mali ya Yawe, kama vile makabila yote ya Israeli yanavyokuwa,


Ujumbe wa neno la Yawe lililowafikia Waisraeli kwa njia ya Malaki.


Malaika wa pili akafuata yule wa kwanza akisema: “Umebomoka, umebomoka kabisa, ule muji mukubwa Babeli. Umewakunywesha mataifa yote divai yake kali, ukiwalewesha na maovu ya uasherati wake.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ