Kwa hiyo, nitawamwangia waadui zangu hasira yangu, nitawalipiza kisasi wapinzani wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi, Mwenye Nguvu wa Israeli.–
Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi anasema hivi: Enyi watu wangu munaokaa Sayuni, musiwaogope Waasuria ambao wanawapiga kwa fimbo, wakiinua gongo zao juu yenu kama walivyofanya Wamisri.
Kisha mwezi utafezeheka, nalo jua litapata haya ya kuangaza, maana Yawe wa majeshi atatawala kule Yerusalema katika mulima Sayuni; ataonyesha wazee wa watu wake utukufu wake.
Enyi watu wa Sayuni, enyi watu wa Yerusalema, hakika ninyi hamutaomboleza tena. Kweli Mungu atawahurumia; mara tu atakaposikia kilio chenu atawaitikia.
Kwenda juu ya mulima murefu, ewe Sayuni, utangaze habari njema. Lalamika kwa nguvu, ewe Yerusalema, utangaze habari njema. Lalamika bila kuogopa. Uambie miji ya Yuda: Muangalie: Mungu wenu!
Mutaipepeta milima hiyo, nao upepo utaipeperushia mbali, zoruba itaitawanya huko na huko. Nanyi mutafurahi kwa sababu yangu Yawe; mutaona utukufu kwa sababu yangu Mungu Mutakatifu wa Israeli.
Nitawasukuma watesaji wako wakule miili yao wenyewe; watalewa damu yao wenyewe kama divai. Halafu wanadamu wote watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mwokozi wako, Mukombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.
Yawe anasema hivi: Imba kwa shangwe, ewe unayekuwa tasa, wewe ambaye haujapata kuzaa! Piga kelele na kuimba kwa nguvu, wewe usiyepata kuzaa mutoto. Maana watoto wako wewe uliyeachwa watakuwa wengi kuliko wa yule anayekuwa na mume.
Utaletewa chakula na watu wa mataifa; wafalme watakupatia chakula bora. Hapo utatambua kwamba mimi Yawe ni Mwokozi wako; mimi Mwenye Nguvu wa Yakobo ni Mukombozi wako.
Wewe ulisema kwamba mataifa hayo mawili, ni kusema inchi ya Yuda na ya Israeli, ni mali yako na kwamba utazirizi! Ulisema hivyo ingawa humo ni makao yangu mimi Yawe.
Nitajulisha jina langu takatifu kwa watu wangu Waisraeli, wala sitaruhusu tena watu walikufuru jina langu takatifu. Nayo mataifa yatatambua kwamba mimi ni Yawe, Mutakatifu wa Israeli.
naye akaniambia: Wewe mwanadamu! Hapa ndipo pahali pa kiti changu cha kifalme, pahali ninapoweka miguu yangu. Nitakaa kati ya watu wa Israeli milele. Na Waisraeli hawatalichafua jina langu, wao wenyewe, wala wafalme wao kwa kuziabudu sanamu au kuzika maiti za wafalme wao pahali hapa.
Kisha eneo la kabila la Yuda, utatenga eneo lenye urefu wa kilometre kumi na mbili na upana kama huohuo, kutoka kaskazini mpaka kusini, na urefu huohuo kutoka mashariki mpaka magaribi, sawasawa na eneo la kabila lolote. Hapo katikati ya eneo hilo patakuwa hekalu la Mungu.
Nitaizuia hasira yangu kali; sitamwangamiza tena Efuraimu, maana mimi ni Mungu, wala si mwanadamu. Mimi ndimi Mutakatifu kati yenu, nami sitakuja kuwaangamiza.
Mutatambua kwamba mimi niko kati yenu, enyi Waisraeli; na kwamba mimi Yawe, ndimi Mungu wenu wala hakuna mwingine. Watu wangu, hawatazarauliwa tena hata kidogo.
Ole wenu wakaaji wa inchi za pembeni ya bahari, watu wanaoishi kule Krete! Yawe amesema juu yenu, enyi wakaaji wa Kanana, inchi ya Wafilistini: Mimi nitawaangamiza wala hakutabaki hata mukaaji mumoja!
Yawe hajaona ubaya kwa watu wa Yakobo, wala uovu kwa hao watu wa Israeli. Yawe Mungu wao yuko pamoja nao, Yeye anasifiwa kwa vigelegele kati yao, yeye anapokea sifa zao za kifalme.
Kambi yenu inapaswa kuwa takatifu kwa sababu Yawe, Mungu wenu anatembea katika kambi yenu kusudi awaokoe na kuwatia waadui zenu katika mikono yenu. Kwa hiyo musimwache aone kitu chochote kisichofaa kati yenu, kama sivyo atawaacha ninyi.