Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 12:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mungu ndiye mwenye kuniokoa, nitamutegemea yeye, wala sitaogopa; Yawe ananijalia nguvu; yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 12:2
41 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata umewaimarisha watu wako Waisraeli kwa ajili yako mwenyewe, kusudi wakuwe watu wako milele; nawe ee Yawe umekuwa Mungu wao.


Kama nikiweza kwa hiyo nitakuwa nimeshinda, maana mutu mwovu hawezi kwenda mbele yake.


Yuko imara ndani ya moyo, wala hataogopa; naye ataona waadui zake wakishindwa.


Yawe ni nguvu yangu kubwa; yeye mwenyewe ndiye wokovu wangu.


Ninakushukuru, ee Yawe, kwa kunijibu; kwa sababu wewe ni wokovu wangu.


Zaburi ya Daudi. Yawe ni mwangaza wangu na wokovu wangu, ni nani nitakayemwogopa? Yawe ni mulinzi wa maisha yangu, sitamwogopa mutu yeyote.


Kwa matendo yako makubwa unatuitikia na kutuokoa, ewe Mungu mwokozi wetu. Wewe ndiwe tumaini la viumbe vyote katika dunia yote na mbali katika bahari.


Yawe asifiwe siku kwa siku! Yeye anatubebea mizigo yetu, yeye ndiye Mungu mwokozi wetu.


Mungu wetu ni Mungu mwenye kutuokoa; Bwana wetu Yawe pekee ndiye anayeokoa katika kifo.


Wafezeheke na kuhangaika milele, waangamie kwa haya kabisa.


Yawe ananijalia nguvu na uwezo, yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa. Yeye ni Mungu wangu nami nitamusifu; ni Mungu wa baba yangu nami nitamutukuza.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi anasema hivi: Enyi watu wangu munaokaa Sayuni, musiwaogope Waasuria ambao wanawapiga kwa fimbo, wakiinua gongo zao juu yenu kama walivyofanya Wamisri.


Maana wewe Israeli umemusahau Mungu aliyekuokoa, haukukumbuka Jiwe lako la kufichamia. Kwa hiyo, hata mukipanda mimea ya Bali, na kuitakasa kwa mungu wa kigeni;


Wakitaka ulinzi wangu, basi, wafanye amani nami. Wafanye amani nami!


Kila mumoja atakuwa kama pahali pa kujikinga na upepo, kama pahali pa kujificha wakati wa mvua kubwa. Watakuwa kama vijito vya maji katika inchi yenye kukauka, kama kivuli cha jiwe kubwa katika jangwa.


Maana Yawe ni mwamuzi wetu, yeye ni mutawala wetu; Yawe ni mufalme wetu, yeye ndiye anayetuokoa.


Yawe ataniokoa. Nasi tutamusifu kwa nyimbo za vinubi siku zote za maisha yetu, katika nyumba ya Yawe.


Lakini taifa la Israeli litaokolewa na Yawe, litapata wokovu wa milele. Halitapata haya wala kuzarauliwa milele.


Lakini sasa Yawe anasema. Aliniita tangu katika tumbo la mama kusudi nipate kuwa mutumishi wake, nilirudishe taifa la Yakobo kwake na kukusanya wazao wa Israeli kwake. Yawe amenijalia heshima mbele yake. Mungu wangu amekuwa nguvu yangu.


Nani kati yenu anayemwogopa Yawe? Nani anayetii maneno ya mutumishi wake? Kama kuna mutu anayetembea katika giza bila taa, amutumainie Yawe, na kumutegemea Mungu wake.


Yawe anasema hivi: Mimi, kweli mimi, ndiye ninayekufariji. Kwa nini wewe unamwogopa mutu ambaye ni wa kufa, mwanadamu ambaye anatoweka kama majani?


Nitafurahi sana kwa sababu ya Yawe, nafsi yangu itashangilia kwa sababu ya Mungu wangu. Maana amenivalisha nguo ya wokovu, amenifunika kanzu ya haki, kama bwana arusi anavyojipamba kwa shada la maua, kama bibi arusi anavyojipamba kwa ushanga wake.


Yawe ametangaza katika dunia yote, muwaambie watu wa Sayuni hivi: Mukombozi wenu anakuja, yeye anakuja na mapato yake, anafika na mushahara wake.


Mufurahi na kushangilia milele, kwa ajili ya vitu hivi ninavyoumba. Yerusalema nitaifanya muji wa shangwe, na watu wake watu wenye furaha.


Basi, Bwana mwenyewe atawapa kitambulisho: bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume na kumwita jina lake “Emanueli – Mungu Yuko Pamoja Nasi”.


Katika siku za utawala wake, inchi ya Yuda itaokolewa na inchi ya Israeli itakuwa katika usalama. Naye ataitwa kwa jina la Yawe Ni Haki Yetu.


Kweli tumedanganyika sana kwa kutambikia huko kwenye vilima, hakika wokovu wa Israeli unatoka kwake Yawe, Mungu wetu.


Basi, mufalme Nebukadneza akasema: Asifiwe Mungu wa Sadiraki, Mesaki na Abedenego kwa sababu alimutuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake ambao wanamutegemea. Wao walikataa kutii amri yangu ya kifalme, wakaitoa miili yao kama sadaka pahali pa kuabudu mungu mwingine, lakini Mungu wao peke yake.


Lakini nitawahurumia watu wa Yuda na kuwaokoa. Mimi Yawe, Mungu wao, nitawaokoa, lakini si kwa nguvu za waaskari, au pinde, au panga, au farasi au waaskari wapanda-farasi.


Mufurahi, enyi watu wa Sayuni, mushangilie kwa sababu ya Yawe, Mungu wenu, maana amewapa mvua zinazowafalia, amewapa mvua ya kutosha: mvua za kwanza na mvua za katikati kama pale mbele.


Watu wanaoabudu sanamu za miungu ya bure, wanautupilia mbali uaminifu wao kwako.


mimi nitaendelea kumufurahia Yawe. Nitamushangilia Mungu anayeniokoa.


Mimi sisikii haya juu ya Habari Njema, kwa sababu huo ndio uwezo wa Mungu unaowaokoa wote wanaoamini, kwanza Wayuda na kisha watu wa mataifa mengine vilevile.


Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.


Nao walilalamika hivi kwa sauti kubwa: “Wokovu wetu unatoka kwa Mungu wetu anayeikaa juu ya kiti cha kifalme na kwa Mwana-Kondoo!”


Halafu Hana aliomba na kusema: Ninamushangilia Yawe ndani ya moyo wangu. Ninamutukuza Yawe anayekuwa nguvu yangu. Ninawachekelea waadui zangu; maana ninaufurahia wokovu wako.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ